< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Job reprit la parole et dit:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Oui, je sais qu’il en est ainsi: comment l’homme aurait-il gain de cause avec Dieu?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
Si nous désirions discuter avec lui, pas une fois sur mille il ne daignerait nous répondre.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Eminemment sage, triomphant de force, qui jamais lui tint tête et s’en trouva bien?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il déplace les montagnes à l’improviste et les bouleverse dans sa colère.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Il fait trembler la terre sur ses bases et ébranle les colonnes qui la supportent.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
II donne un ordre au soleil, et le soleil ne paraît point; il met un sceau sur les étoiles.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
A lui seul, il déploie les cieux; il chemine sur la crête des vagues.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Ila fait la Grande Ourse, l’Orion, les Pléiades et les demeures sidérales du Midi.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Il accomplit des merveilles sans fin, des prodiges qui ne se peuvent compter.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Ah! S’Il passait auprès de moi, je ne le verrais point; s’il se glissait sous mes yeux, je ne le remarquerais pas.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Quand il empoigne quelqu’un, qui lui fera lâcher prise? Qui lui dira: "Que fais-tu?"
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Dieu ne refoule pas sa colère; sous ses coups plient les satellites de l’orgueil.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Et moi j’oserais lui répliquer, je ferais assaut de paroles avec lui,
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
moi, qui tout innocent que je fusse, ne trouverais rien à lui répondre, et demanderais simplement grâce à mon juge!
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Dût-il même se rendre à mon appel, je ne croirais pas qu’il écoute ma voix;
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
car il m’accable sous un vent de tempête et multiplie gratuitement mes blessures.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Il ne me permet pas de reprendre haleine, tant il m’abreuve d’amertumes.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
S’Agit-il de faire preuve de force, il est là! S’Agit-il de jugement, il dira: "Qui pourrait m’assigner?"
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Fussé-je innocent, ma bouche me déclarerait coupable! Fussé-je sans reproche, elle me convaincrait de perversité!
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Oui, je suis sans reproche! Je ne me soucie pas de la vie, je suis las de l’existence.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Tout revient au même: aussi dis-je que juste et méchant, il les fait également périr.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Si un cataclysme entraîne des morts soudaines, il se rit de l’épreuve des innocents.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
Par lui, la terre a été livrée aux impies: il voile les yeux de ceux qui y rendent la justice. Si ce n’est lui, qui serait-ce?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Mes jours sont plus rapides qu’un courrier; ils s’enfuient sans avoir vu le bonheur.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Ils passent comme des barques de jonc, comme l’aigle qui se précipite sur la proie.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Quand je dis: "Je veux oublier ma souffrance, laisser là ma mine attristée et reprendre mes esprits",
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
je suis envahi par la crainte de mes tourments, sachant bien que tu ne m’absoudras pas.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Je serai déclaré coupable: pourquoi donc prendre une peine inutile?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Dussé-je me laver dans de la neige fondue et purifier mes mains avec de la potasse,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
aussitôt tu me plongerais dans une fosse fangeuse, et mes vêtements mêmes auraient horreur de moi.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Car il n’est pas un homme comme moi pour que je lui réponde et que nous paraissions ensemble en justice.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Il n’existe pas d’arbitre entre nous, qui puisse poser sa main sur tous deux.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Qu’il écarte de moi sa verge, et que ses terreurs cessent de peser sur moi.
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Alors je parlerai sans le redouter, car je n’en suis pas là dans le secret de ma conscience.

< Ayubu 9 >