< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Et Job répondit et dit:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
En vérité, je sais qu’il en est ainsi. Mais comment l’homme sera-t-il juste devant Dieu?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
S’il se plaît à contester avec lui, il ne lui répondra pas sur un point entre mille.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Il est sage de cœur et puissant en force: qui s’est endurci contre lui et a prospéré?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il transporte les montagnes, et elles ne savent pas qu’il les renverse dans sa colère;
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Il remue la terre de sa place, et ses colonnes tremblent;
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Il parle au soleil, et [le soleil] ne se lève pas; et sur les étoiles il met son sceau;
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Seul il étend les cieux et marche sur les hauteurs de la mer;
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Il fait la grande Ourse, Orion, et les Pléiades, et les chambres du midi;
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Il fait de grandes choses qu’on ne saurait sonder, et des merveilles à ne pouvoir les compter.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Voici, il passe près de moi, et je ne [le] vois pas; et il passe à côté [de moi], et je ne l’aperçois pas.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Voici, il ravit; qui l’en détournera? Qui lui dira: Que fais-tu?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
Dieu ne retire pas sa colère; sous lui fléchissent les orgueilleux qui prêtent secours.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
Combien moins lui répondrais-je, moi, [et] choisirais-je mes paroles avec lui!
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Si j’étais juste, je ne lui répondrais pas, je demanderais grâce à mon juge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Si je criais, et qu’il me réponde, je ne croirais pas qu’il ait prêté l’oreille à ma voix, –
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Lui qui m’écrase dans une tempête, et qui multiplie mes blessures sans cause.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Il ne me permet pas de reprendre haleine; car il me rassasie d’amertumes.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
S’agit-il de force, voici, il est fort; s’agit-il de jugement: Qui m’assignera?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Si je me justifiais, ma bouche me condamnerait; si j’étais parfait, il me montrerait pervers.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Si j’étais parfait, je méconnaîtrais mon âme, je mépriserais ma vie.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
Tout revient au même; c’est pourquoi j’ai dit: Il consume le parfait et le méchant.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Si le fléau donne subitement la mort, il se rit de l’épreuve de l’innocent.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
La terre est livrée en la main du méchant: il couvre la face de ses juges. S’il n’en est pas ainsi, qui est-ce donc?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
Mes jours s’en vont plus vite qu’un coureur; ils fuient, ils ne voient pas ce qui est bon;
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Ils passent rapides comme les barques de jonc, comme un aigle qui fond sur sa proie.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si je dis: J’oublierai ma plainte, je renoncerai à mon visage [morne] et je serai joyeux,
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Je suis épouvanté de tous mes tourments; je sais que tu ne me tiendras pas pour innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Soit, je suis méchant: pourquoi me fatigué-je ainsi en vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Si je me lave avec de l’eau de neige, et que je nettoie mes mains dans la pureté,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Alors tu me plongeras dans un fossé, et mes vêtements m’auront en horreur.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Car il n’est pas homme, comme moi, pour que je lui réponde, pour que nous allions ensemble en jugement.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Il n’y a pas entre nous un arbitre qui mettrait sa main sur nous deux.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Qu’il retire sa verge de dessus moi, et que sa terreur ne me trouble pas;
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Alors je parlerai et je ne le craindrai pas; mais il n’en est pas ainsi de moi.

< Ayubu 9 >