< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Alors Job répondit,
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
« Je sais en vérité qu'il en est ainsi, mais comment l'homme peut-il être juste avec Dieu?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
S'il lui plaît de contester avec lui, il ne peut pas lui répondre une fois sur mille.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
Dieu est sage de cœur et puissant de force. Qui s'est endurci contre lui et a prospéré?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
Il enlève les montagnes, et ils ne le savent pas, quand il les renverse dans sa colère.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Il secoue la terre de sa place. Ses piliers tremblent.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Il commande au soleil et il ne se lève pas, et scelle les étoiles.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
Lui seul étend les cieux, et marche sur les vagues de la mer.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Il crée l'Ours, Orion et les Pléiades, et les chambres du sud.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Il fait de grandes choses qu'on ne peut pas savoir; oui, des choses merveilleuses sans nombre.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Voici qu'il passe à côté de moi, et je ne le vois pas. Il passe aussi, mais je ne le perçois pas.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Voici qu'il arrache. Qui peut l'en empêcher? Qui lui demandera: « Que fais-tu?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
« Dieu ne retire pas sa colère. Les aides de Rahab s'abaissent sous lui.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
A plus forte raison lui répondrai-je, et choisir mes mots pour argumenter avec lui?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Même si j'étais juste, je n'ai pas voulu lui répondre. Je ferais des supplications à mon juge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Si j'avais appelé, et qu'il m'ait répondu, pourtant je ne croirais pas qu'il ait écouté ma voix.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
Car il me brise par une tempête, et multiplie mes blessures sans raison.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Il ne me permettra pas de reprendre mon souffle, mais me remplit d'amertume.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
Si c'est une question de force, voici qu'il est puissant! S'il s'agit de justice, « Qui, dit-il, me convoquera?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Bien que je sois juste, ma propre bouche me condamne. Bien que je sois irréprochable, cela prouvera ma perversité.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Je suis irréprochable. Je ne me respecte pas. Je méprise ma vie.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
« C'est la même chose. C'est pourquoi je dis qu'il détruit les irréprochables et les méchants.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
Si le fléau tue soudainement, il se moquera du procès des innocents.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
La terre est livrée entre les mains des méchants. Il couvre les visages de ses juges. Si ce n'est pas lui, alors qui est-ce?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
« Maintenant mes jours sont plus rapides qu'un coureur. Ils s'enfuient. Ils ne voient pas le bien.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
Ils ont disparu comme les navires rapides, comme l'aigle qui se jette sur sa proie.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
Si je dis: « J'oublierai ma plainte », J'enlèverai mon visage triste, et je me réjouirai,
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
J'ai peur de tous mes chagrins. Je sais que vous ne me tiendrez pas pour innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
Je serai condamné. Alors pourquoi je travaille en vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
Si je me lave avec de la neige, et je nettoie mes mains avec de la soude,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
pourtant tu me plongeras dans le fossé. Mes propres vêtements me feront horreur.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
Car il n'est pas un homme, comme moi, pour que je lui réponde, que nous devrions nous réunir pour juger.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
Il n'y a pas d'arbitre entre nous, qui pourrait poser sa main sur nous deux.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Qu'il éloigne de moi son bâton. Que sa terreur ne me fasse pas peur;
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
alors je parlerais, et je ne le craindrais pas, car je ne le suis pas en moi-même.

< Ayubu 9 >