< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Of a truth, I know that it is so: For how can man be just before God?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
If he choose to contend with him, He cannot answer him to one charge of a thousand.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
He is excellent in wisdom, mighty in strength: Who hath hardened himself against him, and prospered?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
He removeth the mountains, and they know it not; He overturneth them in his anger.
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
He shaketh the earth out of her place, And the pillars thereof tremble.
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
He commandeth the sun, and it riseth not, And he sealeth up the stars.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
He alone spreadeth out the heavens, And walketh upon the high waves of the sea.
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
He made the Bear, Orion, and the Pleiades, And the secret chambers of the South.
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
He doeth great things past finding out, Yea, wonderful things without number.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
Lo! he goeth by me, but I see him not; He passeth along, but I do not perceive him.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
Lo! he seizeth, and who can hinder him? Who will say to him, What doest thou?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
God will not turn away his anger; The proud helpers are brought low before him.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
How much less shall I answer him, And choose out words to contend with him?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Though I were innocent, I would not answer him; I would cast myself on the mercy of my judge.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
Should I call, and he make answer to me, I could not believe that he listened to my voice, —
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
He who falleth upon me with a tempest, And multiplieth my wounds without cause!
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
Who will not suffer me to take my breath, But filleth me with bitterness!
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
If I look to strength, “Lo! here am I!” [[saith he, ]] If to justice, “Who shall summon me to trial?”
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Though I were upright, yet must my own mouth condemn me; Though I were innocent, He would prove me perverse.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
Though I were innocent, I would not care for myself; I would despise my life.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
It is all one; therefore I will affirm, He destroyeth the righteous and the wicked alike.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
When the scourge bringeth sudden destruction, He laugheth at the sufferings of the innocent.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
The earth is given into the hands of the wicked; He covereth the face of the judges thereof; If it be not He, who is it?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
My days have been swifter than a courier; They have fled away; they have seen no good.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
They have gone by like the reed-skiffs; Like the eagle, darting upon his prey.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
If I say, I will forget my lamentation, I will change my countenance, and take courage,
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
Still am I in dread of the multitude of my sorrows; For I know that thou wilt not hold me innocent.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
I shall be found guilty; Why then should I labor in vain?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
If I wash myself in snow, And cleanse my hands with lye,
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Still wilt thou plunge me into the pit, So that my own clothes will abhor me.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
For He is not a man, as I am, that I may contend with him, And that we may go together into judgment;
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
There is no umpire between us, Who may lay his hand upon us both.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Let him take from me his rod, And not dismay me with his terrors,
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Then I will speak, and not be afraid of him: For I am not so at heart.

< Ayubu 9 >