< Ayubu 9 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
And Job made answer and said,
2 “kweli najua kwamba ndivyo hivyo. Lakini ni kwa namna gani mtu anakuwa na haki kwa Mungu?
Truly, I see that it is so: and how is it possible for a man to get his right before God?
3 Kama akitaka kujibishana na Mungu, hatamjibu yeye mara moja katika elfu zaidi.
If a man was desiring to go to law with him, he would not be able to give him an answer to one out of a thousand questions.
4 Mungu ni mwenye hekima moyoni na ukuu katika nguvu; ni nani daima aliyejifanya mwenyewe kuwa mgumu dhidi yake na akafanikiwa? -
He is wise in heart and great in strength: who ever made his face hard against him, and any good came of it?
5 ambaye huiondoa milima bila kumtahadharisha yeyote wakati akiipindua katika hasira zake -
It is he who takes away the mountains without their knowledge, overturning them in his wrath:
6 ambaye huitikisa nchi itoke mahali pake na mihimili yake hutikisika.
Who is moving the earth out of its place, so that its pillars are shaking:
7 Ni Mungu yule yule ambaye huliamuru jua lisichomoze, nalo halichomozi, na ambaye huzihifadhi nyota,
Who gives orders to the sun, and it does not give its light; and who keeps the stars from shining.
8 ambaye peke yake ni mwenye kupanua mbingu na kuyatuliza mawimbi ya bahari,
By whose hand the heavens were stretched out, and who is walking on the waves of the sea:
9 ambaye huumba Dubu, Orioni, kilima, na makundi ya nyota ya kusini.
Who made the Bear and Orion, and the Pleiades, and the store-houses of the south:
10 Ni Mungu yule yule atendaye mambo makuu, mambo yasiyofahamika - hasa, mambo ya ajabu yasiyohesabika.
Who does great things not to be searched out; yes, wonders without number.
11 Tazama, huenda karibu nami, na siwezi kumuona yeye; pia hupita kwenda mbele, lakini ni simtambue.
See, he goes past me and I see him not: he goes on before, but I have no knowledge of him.
12 Kama akichukua kitu chochote, nani atamzuia? Nani awezaye kumuuliza, 'unafanya nini?'
If he puts out his hand to take, by whom may it be turned back? who may say to him, What are you doing?
13 Mungu hataondoa hasira yake; wamsaidiao Rahabu huinama chini yake.
God's wrath may not be turned back; the helpers of Rahab were bent down under him.
14 Je ni upungufu kiasi gani mimi nitamjibu, je nichague maneno kuhojiana naye?
How much less may I give an answer to him, using the right words in argument with him?
15 Hata kama ni mwenye haki, nisingelimjibu; ningeomba msamaha tu kwa hukumu yangu.
Even if my cause was good, I would not be able to give an answer; I would make request for grace from him who was against me.
16 Hata kama ningelimwita na yeye akanitikia, nisingeamini kuwa ameisikia sauti yangu.
If I had sent for him to be present, and he had come, I would have no faith that he would give ear to my voice.
17 kwa kuwa yeye anidhoofishaye kwa dhoruba na kuyaongeza majeraha yangu pasipo sababu.
For I would be crushed by his storm, my wounds would be increased without cause.
18 Yeye hataki hata kuniruhusu nipate kuvuta pumzi; badala yake, hunijaza uchungu.
He would not let me take my breath, but I would be full of bitter grief.
19 Kama ni habari ya nguvu, tazama! yeye ni mwenye uwezo! Kama ni habari ya haki, ni nani atakaye mhukumu?
If it is a question of strength, he says, Here I am! and if it is a question of a cause at law, he says, Who will give me a fixed day?
20 Ingawa ni mwenye haki, kinywa changu mwenyewe kitanihukumu; na ingawa ni mtakatifu, maneno yangu yatashuhudia kuwa ni mwenye kosa.
Though I was in the right, he would say that I was in the wrong; I have done no evil; but he says that I am a sinner.
21 Mimi ni mtakatifu, lakini siijali zaidi nafsi yangu; Naudharau uhai wangu mwenyewe.
I have done no wrong; I give no thought to what becomes of me; I have no desire for life.
22 Haileti tofauti yoyote, kwa sababu hiyo nasema kwamba yeye huangamiza watu wasio na makosa na waovu pia.
It is all the same to me; so I say, He puts an end to the sinner and to him who has done no wrong together.
23 Kama hilo pigo likiua ghafla, yeye atafurahi mateso yake mtu asiye na kosa.
If death comes suddenly through disease, he makes sport of the fate of those who have done no wrong.
24 Dunia imetiwa mkononi mwa watu waovu; Mungu hufunika nyuso za waamuzi wake. kama si yeye hufanya, ni nani basi?
The land is given into the power of the evil-doer; the faces of its judges are covered; if not by him, then who has done it?
25 Siku zangu zinapita haraka kuliko tarishi akimbiae; siku zangu zinakimbia mbali; wala hazioni mema mahali popote.
My days go quicker than a post-runner: they go in flight, they see no good.
26 Zinapita kama mashua zilizoundwa kwa mafunjo ziendazo kwa kasi, na zinakasi kama tai ashukaye upesi katika mawindo yake.
They go rushing on like reed-boats, like an eagle dropping suddenly on its food.
27 Kama ni kisema kwamba mimi nitasahau kuhusu manung'uniko yangu, kwamba nitaacha kuonyesha sura ya huzuni na kuwa na furaha,
If I say, I will put my grief out of mind, I will let my face be sad no longer and I will be bright;
28 Mimi nitaziogopa huzuni zangu zote kwa sababu nafahamu kuwa hutanihesabu kuwa sina hatia.
I go in fear of all my pains; I am certain that I will not be free from sin in your eyes.
29 Nitahukumiwa; kwa nini, basi, nitaabike bure?
You will not let me be clear of sin! why then do I take trouble for nothing?
30 Kama najiosha mwenyewe kwa maji ya theluji na kuitakasa mikono yangu na kuwa safi zaidi,
If I am washed with snow water, and make my hands clean with soap;
31 Mungu atanitumbukiza shimoni, na nguo zangu mwenyewe zitanichukia.
Then you will have me pushed into the dust, so that I will seem disgusting to my very clothing.
32 Kwa kuwa Mungu si mtu, kama mimi, kwamba naweza kumjibu, hata tukaribiane katika hukumu.
For he is not a man as I am, that I might give him an answer, that we might come together before a judge.
33 Hakuna hakimu baina yetu awezaye kuweka mkono wake juu yetu sote.
There is no one to give a decision between us, who might have control over us.
34 Hakuna hakimu mwingine ambaye anaweza kuniondolea fimbo ya Mungu, awezaye kuzuia kitisho chake kisinitie hofu. kisha ningesema na nisimuogope.
Let him take away his rod from me and not send his fear on me:
35 Lakini kama mambo yalivyo sasa, sitaweza kufanya hivyo.
Then I would say what is in my mind without fear of him; for there is no cause of fear in myself.

< Ayubu 9 >