< Ayubu 8 >
1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
respondens autem Baldad Suites dixit
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
usquequo loqueris talia et spiritus multiplex sermones oris tui
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
numquid Deus subplantat iudicium et Omnipotens subvertit quod iustum est
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
etiam si filii tui peccaverunt ei et dimisit eos in manu iniquitatis suae
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
tu tamen si diluculo consurrexeris ad Deum et Omnipotentem fueris deprecatus
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
si mundus et rectus incesseris statim evigilabit ad te et pacatum reddet habitaculum iustitiae tuae
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
in tantum ut priora tua fuerint parva et novissima tua multiplicentur nimis
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
interroga enim generationem pristinam et diligenter investiga patrum memoriam
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
hesterni quippe sumus et ignoramus quoniam sicut umbra dies nostri sunt super terram
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
et ipsi docebunt te loquentur tibi et de corde suo proferent eloquia
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
numquid vivere potest scirpus absque humore aut crescet carectum sine aqua
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
cum adhuc sit in flore nec carpatur manu ante omnes herbas arescit
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
sic viae omnium qui obliviscuntur Deum et spes hypocritae peribit
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
non ei placebit vecordia sua et sicut tela aranearum fiducia eius
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
innitetur super domum suam et non stabit fulciet eam et non consurget
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
humectus videtur antequam veniat sol et in horto suo germen eius egreditur
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
super acervum petrarum radices eius densabuntur et inter lapides commorabitur
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
si absorbuerit eum de loco suo negabit eum et dicet non novi te
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
haec est enim laetitia viae eius ut rursum de terra alii germinentur
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Deus non proiciet simplicem nec porriget manum malignis
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
donec impleatur risu os tuum et labia tua iubilo
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
qui oderunt te induentur confusione et tabernaculum impiorum non subsistet