< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
수아 사람 빌닷이 대답하여 가로되
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
네가 어느 때까지 이런 말을 하겠으며 어느 때까지 네 입의 말이 광풍과 같겠는가
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
하나님이 어찌 심판을 굽게 하시겠으며 전능하신이가 어찌 공의를 굽게 하시겠는가
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
네 자녀들이 주께 득죄하였으므로 주께서 그들을 그 죄에 붙이셨나니
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
네가 만일 하나님을 부지런히 구하며 전능하신 이에게 빌고
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
또 청결하고 정직하면 정녕 너를 돌아보시고 네 의로운 집으로 형통하게 하실 것이라
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
네 시작은 미약하였으나 네 나중은 심히 창대하리라
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
청컨대 너는 옛시대 사람에게 물으며 열조의 터득한 일을 배울지어다
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(우리는 어제부터 있었을 뿐이라 지식이 망매하니 세상에 있는 날이 그림자와 같으니라)
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
그들이 네게 가르쳐 이르지 아니하겠느냐 그 마음에서 나는 말을 발하지 아니하겠느냐
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
왕골이 진펄이 아니고 나겠으며 갈대가 물 없이 자라겠느냐
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
이런 것은 푸르러도 아직 벨 때 되기 전에 다른 풀보다 일찌기 마르느니라
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
하나님을 잊어버리는 자의 길은 다 이와 같고 사곡한 자의 소망은 없어지리니
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
그 믿는 것이 끊어지고 그 의지하는 것이 거미줄 같은즉
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
그 집을 의지할지라도 집이 서지 못하고 굳게 잡아도 집이 보존 되지 못하리라
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
식물이 일광을 받고 푸르러서 그 가지가 동산에 벋어가며
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
그 뿌리가 돌 무더기에 서리어서 돌 가운데로 들어 갔을지라도
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
그 곳에서 뽑히면 그 자리도 모르는 체하고 이르기를 내가 너를 보지 못하였다 하리니
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
그 길의 희락은 이와 같고 그 후에 다른 것이 흙에서 나리라
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
하나님은 순전한 사람을 버리지 아니하시고 악한 자를 붙들어 주지 아니하신즉
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
웃음으로 네 입에, 즐거운 소리로 네 입술에 채우시리니
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
너를 미워하는 자는 부끄러움을 입을 것이라 악인의 장막은 없어지리라

< Ayubu 8 >