< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
ויען בלדד השוחי ויאמר׃
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
עד אן תמלל אלה ורוח כביר אמרי פיך׃
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
האל יעות משפט ואם שדי יעות צדק׃
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
אם בניך חטאו לו וישלחם ביד פשעם׃
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
אם אתה תשחר אל אל ואל שדי תתחנן׃
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
אם זך וישר אתה כי עתה יעיר עליך ושלם נות צדקך׃
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
והיה ראשיתך מצער ואחריתך ישגה מאד׃
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
כי שאל נא לדר רישון וכונן לחקר אבותם׃
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
כי תמול אנחנו ולא נדע כי צל ימינו עלי ארץ׃
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
הלא הם יורוך יאמרו לך ומלבם יוצאו מלים׃
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
היגאה גמא בלא בצה ישגה אחו בלי מים׃
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
עדנו באבו לא יקטף ולפני כל חציר ייבש׃
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
כן ארחות כל שכחי אל ותקות חנף תאבד׃
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
אשר יקוט כסלו ובית עכביש מבטחו׃
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
ישען על ביתו ולא יעמד יחזיק בו ולא יקום׃
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
רטב הוא לפני שמש ועל גנתו ינקתו תצא׃
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
על גל שרשיו יסבכו בית אבנים יחזה׃
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
אם יבלענו ממקומו וכחש בו לא ראיתיך׃
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
הן הוא משוש דרכו ומעפר אחר יצמחו׃
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
הן אל לא ימאס תם ולא יחזיק ביד מרעים׃
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
עד ימלה שחוק פיך ושפתיך תרועה׃
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
שנאיך ילבשו בשת ואהל רשעים איננו׃

< Ayubu 8 >