< Ayubu 8 >
1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Bildad de Schuach prit la parole et dit:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Jusqu’à quand veux-tu discourir de la sorte, Et les paroles de ta bouche seront-elles un vent impétueux?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Dieu renverserait-il le droit? Le Tout-Puissant renverserait-il la justice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Si tes fils ont péché contre lui, Il les a livrés à leur péché.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Mais toi, si tu as recours à Dieu, Si tu implores le Tout-Puissant;
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
Si tu es juste et droit, Certainement alors il veillera sur toi, Et rendra le bonheur à ton innocente demeure;
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
Ton ancienne prospérité semblera peu de chose, Celle qui t’est réservée sera bien plus grande.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Interroge ceux des générations passées, Sois attentif à l’expérience de leurs pères.
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
Car nous sommes d’hier, et nous ne savons rien, Nos jours sur la terre ne sont qu’une ombre.
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Ils t’instruiront, ils te parleront, Ils tireront de leur cœur ces sentences:
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Le jonc croît-il sans marais? Le roseau croît-il sans humidité?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Encore vert et sans qu’on le coupe, Il sèche plus vite que toutes les herbes.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Ainsi arrive-t-il à tous ceux qui oublient Dieu, Et l’espérance de l’impie périra.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Son assurance est brisée, Son soutien est une toile d’araignée.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
Il s’appuie sur sa maison, et elle n’est pas ferme; Il s’y cramponne, et elle ne résiste pas.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
Dans toute sa vigueur, en plein soleil, Il étend ses rameaux sur son jardin,
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
Il entrelace ses racines parmi les pierres, Il pénètre jusque dans les murailles;
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
L’arrache-t-on du lieu qu’il occupe, Ce lieu le renie: Je ne t’ai point connu!
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
Telles sont les délices que ses voies lui procurent. Puis sur le même sol d’autres s’élèvent après lui.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Non, Dieu ne rejette point l’homme intègre, Et il ne protège point les méchants.
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Il remplira ta bouche de cris de joie, Et tes lèvres de chants d’allégresse.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
Tes ennemis seront couverts de honte; La tente des méchants disparaîtra.