< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Et Baldad de Sauchée répondant dit:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Jusqu'à quand parleras-tu de la sorte? Quel esprit verbeux s'exprime par ta bouche?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Dieu est-il un juge prévaricateur? Le créateur de toutes choses torture-t- il l'équité?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Si tes fils ont péché devant lui, il leur a, de sa main, fait expier leurs fautes.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Commence donc dès l'aurore à prier le Seigneur tout-puissant.
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
Si tu es pur et sincère, il t'exaucera et il te traitera selon sa justice.
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
Ce que tu possédais d'abord te semblera médiocre; ce que tu posséderas finalement sera inexprimable.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Remonte jusqu'à la première génération; suit à la trace les générations de nos pères.
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
Car nous sommes d'hier et nous ne savons rien; notre vie sur la terre est une ombre.
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
N'est-ce donc pas à nos pères de t'instruire, de t'éclairer, et de tirer de leur cœur les paroles que je vais dire?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Le papyrus croît-il sans eau? L'herbe des prairies pousse-t-elle si elle n'est pas arrosée?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
La fauche-t-on quand elle est encore près de la racine? Et la plante que rien n'abreuve ne dessèche-t-elle pas?
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Ainsi finissent ceux que le Seigneur oublie, car l'espérance de l'impie est vaine.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Sa maison sera déserte; sa tente disparaîtra comme une toile d'araignée.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
Il aura beau l'étayer, elle ne sera pas solide; dès qu'il en sera enlevé, elle s'écroulera.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
Il y a de l'humidité sous le soleil, une tige sort de la moisissure qu'elle engendre.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
Elle s'élève sur un tas de pierres; elle subsiste au milieu des cailloux.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
Et s'ils viennent à la dévorer, le lieu même se prêtera à nier son existence. N'as-tu pas vu pareille chose?
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
N'est-ce pas comme cette tige que succombe l'impie? Une autre plante hors de terre germera.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Jamais le Seigneur ne rejettera l'innocence; il n'acceptera pas les dons des pervers.
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Il mettra le sourire sur les lèvres des hommes sincères, et leur bouche sera pleine de ses louanges.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
Leurs ennemis seront couverts de honte; et il n'y aura pas de vie heureuse pour les méchants.

< Ayubu 8 >