< Ayubu 8 >
1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Et Bildad, le Shukhite, répondit et dit:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Jusques à quand diras-tu ces choses, et les paroles de ta bouche seront-elles un vent impétueux?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Est-ce que Dieu pervertit le droit? Le Tout-puissant pervertira-t-il la justice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Si tes fils ont péché contre lui, il les a aussi livrés en la main de leur transgression.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Si tu recherches Dieu et que tu supplies le Tout-puissant,
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
Si tu es pur et droit, certainement il se réveillera maintenant en ta faveur, et rendra prospère la demeure de ta justice;
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
Et ton commencement aura été petit, mais ta fin sera très grande.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Car interroge, je te prie, la génération précédente, et sois attentif aux recherches de leurs pères;
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
Car nous sommes d’hier et nous n’avons pas de connaissance, car nos jours sont une ombre sur la terre.
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Ceux-là ne t’enseigneront-ils pas, ne te parleront-ils pas, et de leurs cœurs ne tireront-ils pas des paroles?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Le papyrus s’élève-t-il où il n’y a pas de marais? Le roseau croît-il sans eau?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Encore dans sa verdeur, sans qu’on l’ait arraché, avant toute herbe il sèche.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Tels sont les sentiers de tous ceux qui oublient Dieu; et l’attente de l’impie périra;
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Son assurance sera retranchée, et sa confiance sera une toile d’araignée:
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
Il s’appuiera sur sa maison, et elle ne tiendra pas; il s’y cramponnera, et elle ne restera pas debout.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
Il est verdoyant devant le soleil, et son rameau s’étend sur son jardin;
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
Ses racines s’entrelacent dans un tas de rocaille, il voit la demeure des pierres;
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
S’Il l’ôte de sa place, celle-ci le désavouera: Je ne t’ai pas vu!
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
Telles sont les délices de ses voies; et de la poussière, d’autres germeront.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Voici, Dieu ne méprisera pas l’homme parfait, et ne soutiendra pas les mains des méchants:
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Tandis qu’il remplira ta bouche de rire et tes lèvres de chants de joie,
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
Ceux qui te haïssent seront revêtus de honte, et la tente des méchants ne sera plus.