< Ayubu 8 >
1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Then answered Bildad the Shuhite, and said,
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
How long wilt thou speak these things? and [how long] shall the words of thy mouth be [like] a mighty wind?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Doth God pervert judgment? or doth the Almighty pervert justice?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
If thy children have sinned against him, and he have delivered them into the hand of their transgression:
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
If thou wouldest seek diligently unto God, and make thy supplication to the Almighty;
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
If thou wert pure and upright; surely now he would awake for thee, and make the habitation of thy righteousness prosperous.
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
And though thy beginning was small, yet thy latter end should greatly increase.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
For inquire, I pray thee, of the former age, and apply thyself to that which their fathers have searched out:
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(For we are but of yesterday, and know nothing, because our days upon earth are a shadow: )
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Shall not they teach thee, and tell thee, and utter words out of their heart?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Can the rush grow up without mire? can the flag grow without water?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Whilst it is yet in its greenness, [and] not cut down, it withereth before any [other] herb.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
So are the paths of all that forget God; and the hope of the godless man shall perish:
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Whose confidence shall break in sunder, and whose trust is a spider’s web.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
He shall lean upon his house, but it shall not stand: he shall hold fast thereby, but it shall not endure.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
He is green before the sun, and his shoots go forth over his garden.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
His roots are wrapped about the heap, he beholdeth the place of stones.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
If he be destroyed from his place, then it shall deny him, [saying], I have not seen thee.
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
Behold, this is the joy of his way, and out of the earth shall others spring.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Behold, God will not cast away a perfect man, neither will he uphold the evil-doers.
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
He will yet fill thy mouth with laughter, and thy lips with shouting.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
They that hate thee shall be clothed with shame; and the tent of the wicked shall be no more.