< Ayubu 8 >

1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
The Baldad the Suhite answered, and said:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
How long wilt thou speak these things, and how long shall the words of thy mouth be like a strong wind?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Doth God pervert judgment, or doth the Almighty overthrow that which is just?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Although thy children have sinned against him, and he hath left them in the hand of their iniquity:
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Yet if thou wilt arise early to God, and wilt beseech the Almighty:
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
If thou wilt walk clean and upright, he will presently awake onto thee, and will make the dwelling of thy justice peaceable:
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
Insomuch, that if thy former things were small, thy latter things would be multiplied exceedingly.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
For inquire of the former generation, and search diligently into the memory of the fathers:
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(For we are but of yesterday, and are ignorant that our days upon earth are but a shadow: )
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
And they shall teach thee: they shall speak to thee, and utter words out of their hearts.
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Can the rush be green without moisture? or a sedge-bush grow without water?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
When it is yet in flower, and is not plucked up with the hand, it withereth before all herbs.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Even so are the ways of all that forget God, and the hope of the hypocrite shall perish:
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
His folly shall not please him, and his trust shall be like the spider’s web.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
He shall lean upon his house, and it shall not stand: he shall prop it up, and it shall not rise:
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
He seemeth to have moisture before the sun cometh, and at his rising his blossom shall shoot forth.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
His roots shall be thick upon a heap of stones, and among the stones he shall abide.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
If one swallow him up out of his place, he shall deny him, and shall say: I know thee not.
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
For this is the joy of his way, that others may spring again out of the earth.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
God will not cast away the simple, nor reach out his hand to the evildoer:
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Until thy mouth be filled with laughter, and thy lips with rejoicing.
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
They that hate thee, shall be clothed with confusion: and the dwelling of the wicked shall not stand.

< Ayubu 8 >