< Ayubu 8 >
1 Kisha Bildadi huyo Mshuhi akajibu na kusema,
Tedy odpovídaje Bildad Suchský, řekl:
2 “hata lini wewe utasema mambo haya? Kwa muda gani maneno ya kinywa chako yatakuwa kama upepo wenye nguvu?
Dokudž mluviti budeš takové věci, a slova úst tvých budou jako vítr násilný?
3 Je Mungu hupotosha hukumu? Je Mwenyezi hupotosha haki?
Což by Bůh silný neprávě soudil, a Všemohoucí což by převracel spravedlnost?
4 Watoto wako wametenda dhambi dhidi yake; tunalifahamu hili, kwa kuwa amewatia mkononi kwa makosa yao.
Synové zajisté tvoji že zhřešili proti němu, proto pustil je po nepravosti jejich.
5 Lakini wewe unaonaje ukimtafuta Mungu kwa bidii na kufikisha haja yako kwa huyo Mwenyezi.
Kdybys ty opravdově hledal Boha silného, a Všemohoucímu se modlil,
6 Ukiwa wewe ni msafi na mkamilifu, hakika angeamka mwenyewe kwa niaba yako na kukurudisha kwenye makazi ya haki yako.
A byl čistý a upřímý: jistě žeť by se hned probudil k tobě, a napravil by příbytek spravedlnosti tvé.
7 Japokuwa huo mwanzo wako ulikuwa ni mdogo, hata hivyo hali yako ya mwisho itaongezeka sana.
A byly by první věci tvé špatné, poslední pak rozmnožily by se náramně.
8 Tafadhari uwaulize vizazi vya zamani, na utie bidii katika hayo mababu zetu waliyojifunza.
Nebo vzeptej se, prosím, věku starého, a nastroj se k zpytování otců jejich.
9 (Sisi ni wa jana tu na hatujui chochote kwa kuwa siku zetu duniani ni kivuli).
(Myť zajisté včerejší jsme, aniž jsme čeho povědomi; k tomu dnové naši jsou jako stín na zemi.)
10 Je hawatakufunza wao na kukuambia? Je hawatatamka maneno yatokayo mioyoni mwao?
Zdaliž tě oni nenaučí, a nepovědí tobě, a z srdce svého nevynesou-liž slov?
11 Je hayo mafunjo yaota pasipo matope? Je mafunjo yaota pasipo maji?
Zdali roste třtí bez bahna? Roste-liž rákosí bez vody?
12 Wakati yakiwa bado ya kijani na hayajakatwa, hunyauka kabla ya mmea mwingine.
Nýbrž ještě za zelena, dříve než vytrháno bývá, ano prvé než jaká jiná tráva, usychá.
13 Hivyo pia njia ya wote wamsahauo Mungu, na matumaini ya asiyeamini Mungu yatatoweka.
Tak stezky všech zapomínajících se na Boha silného, tak, pravím, naděje pokrytce zahyne.
14 Ujasiri wake utavunjika, na matumaini yake ni dhaifu kama utando wa buibui.
Klesne naděje jeho, a doufání jeho jako dům pavouka.
15 Ataitegemea nyumba yake, lakini haitamsaidia; atashikamana nayo, lakini isidumu.
Spolehne-li na dům svůj, neostojí; chytí-li se ho, nezdrží.
16 Yeye huwa mti mbichi chini ya jua, na machipukizi yake huenea katika bustani yake yote.
Vláhu má před sluncem, tak že z zahrady jeho výstřelkové jeho vynikají.
17 Mizizi yake hujifunga funga kwenye rundo la mawe; huangalia mahali pazuri katikati ya mawe;
Při vrchovišti kořenové jeho hustě rostou, i na místech skalnatých rozkládá se.
18 Lakini mtu huyu aking'olewa mahali pake, kisha mahali pale patamkana, na kusema, 'mimi sikukuona.'
A však bývá-li zachvácen z místa svého, až by se ho i odečtlo, řka: Nevidělo jsem tě:
19 Tazama, hii ni “furaha” ya mtu mwenye tabia hiyo; mimea mingine itachipuka toka katika udongo ule ule mahali pake.
Tožť ta radost života jeho, a z země jiný vykvetá.
20 Tazama, Mungu hatamtupa mtu asiye na kosa; wala hatawathibitisha watendao uovu.
Aj, Bůh silný nepohrdá upřímým, ale nešlechetným ruky nepodává:
21 Yeye atakijaza kinywa chako na kicheko, midomo yako na shangwe.
Až i naplní smíchem ústa tvá, a rty tvé plésáním,
22 Wale ambao wanakuchukia wewe watavishwa aibu; nayo hema yake mwovu haitakuwepo tena.
Když nenávidící tebe v hanbu oblečeni budou, a stánku lidí bezbožných nikdež nebude.