< Ayubu 7 >
1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
Milicia es la vida del hombre sobre la tierra; como los del jornalero son sus días.
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
Como el siervo suspira por la sombra, y como el jornalero espera su salario;
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
así heredé meses de calamidad, y noches de dolor me tocaron en suerte.
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
Si me acuesto, digo: “¿Cuándo me levantaré?” Mas la noche es larga, y me canso, dándome vuelta hasta el alba.
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
Mi carne está cubierta de gusanos y de una costra de barro; mi piel se rompe y se deshace.
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
Mis días pasan más ligeros que la lanzadera, y desaparecen sin esperanza.
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
Acuérdate de que mi vida es un soplo; mis ojos ya no verán la felicidad.
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
No me verá más el ojo del que ahora me ve; apenas tus ojos me ven, y ya no subsisto.
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol )
La nube se disipa y pasa; así no sube más el que desciende al sepulcro. (Sheol )
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
No volverá más a su casa, ni le reconocerá su lugar.
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
Por eso, no refrenaré mi lengua, hablaré en la angustia de mi espíritu, me quejaré en la amargura de mi alma.
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
¿Soy yo el mar, o algún monstruo marino, para que me tengas encerrado con guardias?
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
Cuando digo: Mi lecho me consolará, mi cama aliviará mi pesar,
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
entonces me aterras con sueños, y me espantas con visiones.
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
Por eso prefiero ser ahogado, deseo la muerte para estos mis huesos.
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
Tengo asco; no quiero vivir más; déjame, ya que mi vida es un soplo.
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
¿Qué es el hombre, para que tanto le estimes, y fijes en él tu atención,
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
para que le visites cada mañana, y a cada momento le pruebes?
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
¿Cuándo cesarás de mirarme, y me das tiempo para tragar mi saliva?
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
Si he pecado, ¿qué te he hecho con eso, oh Guardador de los hombres? ¿Por qué me pones por blanco a mí, que soy una carga para mí mismo?
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
¿Por qué no perdonas mi pecado ni borras mi iniquidad? Pues pronto me dormiré en el polvo; y si me buscas, ya no existiré.”