< Ayubu 7 >

1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
militia est vita hominis super terram et sicut dies mercennarii dies eius
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
sicut servus desiderat umbram et sicut mercennarius praestolatur finem operis sui
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
sic et ego habui menses vacuos et noctes laboriosas enumeravi mihi
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
si dormiero dico quando consurgam et rursum expectabo vesperam et replebor doloribus usque ad tenebras
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
induta est caro mea putredine et sordibus pulveris cutis mea aruit et contracta est
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
dies mei velocius transierunt quam a texente tela succiditur et consumpti sunt absque ulla spe
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
memento quia ventus est vita mea et non revertetur oculus meus ut videat bona
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
nec aspiciet me visus hominis oculi tui in me et non subsistam
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol h7585)
sicut consumitur nubes et pertransit sic qui descenderit ad inferos non ascendet (Sheol h7585)
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
nec revertetur ultra in domum suam neque cognoscet eum amplius locus eius
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
quapropter et ego non parcam ori meo loquar in tribulatione spiritus mei confabulabor cum amaritudine animae meae
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
numquid mare sum ego aut cetus quia circumdedisti me carcere
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
si dixero consolabitur me lectulus meus et relevabor loquens mecum in strato meo
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
terrebis me per somnia et per visiones horrore concuties
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
quam ob rem elegit suspendium anima mea et mortem ossa mea
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
desperavi nequaquam ultra iam vivam parce mihi nihil enim sunt dies mei
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
quid est homo quia magnificas eum aut quia ponis erga eum cor tuum
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
visitas eum diluculo et subito probas illum
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
usquequo non parces mihi nec dimittis me ut gluttiam salivam meam
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
peccavi quid faciam tibi o custos hominum quare posuisti me contrarium tibi et factus sum mihimet ipsi gravis
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
cur non tolles peccatum meum et quare non auferes iniquitatem meam ecce nunc in pulvere dormiam et si mane me quaesieris non subsistam

< Ayubu 7 >