< Ayubu 7 >

1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
Non ha forse un duro lavoro l'uomo sulla terra e i suoi giorni non sono come quelli d'un mercenario?
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
Come lo schiavo sospira l'ombra e come il mercenario aspetta il suo salario,
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
così a me son toccati mesi d'illusione e notti di dolore mi sono state assegnate.
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
Se mi corico dico: «Quando mi alzerò?». Si allungano le ombre e sono stanco di rigirarmi fino all'alba.
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
Ricoperta di vermi e croste è la mia carne, raggrinzita è la mia pelle e si disfà.
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
I miei giorni sono stati più veloci d'una spola, sono finiti senza speranza.
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
Ricordati che un soffio è la mia vita: il mio occhio non rivedrà più il bene.
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
Non mi scorgerà più l'occhio di chi mi vede: i tuoi occhi saranno su di me e io più non sarò.
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol h7585)
Una nube svanisce e se ne va, così chi scende agl'inferi più non risale; (Sheol h7585)
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
non tornerà più nella sua casa, mai più lo rivedrà la sua dimora.
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
Ma io non terrò chiusa la mia bocca, parlerò nell'angoscia del mio spirito, mi lamenterò nell'amarezza del mio cuore!
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
Son io forse il mare oppure un mostro marino, perché tu mi metta accanto una guardia?
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
Quando io dico: «Il mio giaciglio mi darà sollievo, il mio letto allevierà la mia sofferenza»,
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
tu allora mi spaventi con sogni e con fantasmi tu mi atterrisci.
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
Preferirei essere soffocato, la morte piuttosto che questi miei dolori!
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
Io mi disfaccio, non vivrò più a lungo. Lasciami, perché un soffio sono i miei giorni.
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
Che è quest'uomo che tu nei fai tanto conto e a lui rivolgi la tua attenzione
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
e lo scruti ogni mattina e ad ogni istante lo metti alla prova?
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
Fino a quando da me non toglierai lo sguardo e non mi lascerai inghiottire la saliva?
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
Se ho peccato, che cosa ti ho fatto, o custode dell'uomo? Perché m'hai preso a bersaglio e ti son diventato di peso?
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
Perché non cancelli il mio peccato e non dimentichi la mia iniquità? Ben presto giacerò nella polvere, mi cercherai, ma più non sarò!

< Ayubu 7 >