< Ayubu 7 >
1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
Is there not a war-service for man on the earth? Are not his days as the days of a hireling?
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
As a servant panteth for the shade, And as a hireling looketh for his wages,
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
So am I made to possess months of affliction, And wearisome nights are appointed for me.
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
If I lie down, I say, When shall I arise, and the night be gone? And I am full of restlessness until the dawning of the day.
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
My flesh is clothed with worms, and clods of dust; My skin is broken and become loathsome.
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
My days are swifter than a weaver's shuttle; They pass away without hope.
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
O remember that my life is a breath; That mine eye shall no more see good!
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
The eye of him that hath seen me shall see me no more; Thine eyes shall look for me, but I shall not be.
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol )
As the cloud dissolveth and wasteth away, So he that goeth down to the grave shall arise no more; (Sheol )
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
No more shall he return to his house, And his dwelling-place shall know him no more.
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
Therefore I will not restrain my mouth; I will speak in the anguish of my spirit; I will complain in the bitterness of my soul.
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
Am I a sea, or a sea-monster, That thou settest a watch over me?
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
When I say, My bed shall relieve me, My couch shall ease my complaint,
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
Then thou scarest me with dreams, And terrifiest me with visions;
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
So that my soul chooseth strangling, Yea, death, rather than these my bones.
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
I am wasting away; I shall not live alway: Let me alone, for my days are a vapor!
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
What is man, that thou shouldst make great account him, And fix thy mind upon him?—
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
That thou shouldst visit him every morning, And prove him every moment?
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
How long ere thou wilt look away from me, And let me alone, till I have time to breathe?
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
If I have sinned, what have I done to thee, O thou watcher of men! Why hast thou set me up as thy mark, So that I have become a burden to myself?
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
And why dost thou not pardon my transgression, And take away mine iniquity? For soon shall I sleep in the dust; And, though thou seek me diligently, I shall not be.