< Ayubu 7 >

1 Je mtu hana kazi ngumu juu ya nchi? Je siku zake si kama siku za mwajiriwa?
人在世上岂无争战吗? 他的日子不像雇工人的日子吗?
2 Kama mtumwa atamaniye sana kivuli cha jioni, kama mwajiriwa atafutaye ujira wake -
像奴仆切慕黑影, 像雇工人盼望工价;
3 hivyo nami nimeumbwa kuvumilia miezi ya taabu; Nami nimepewa taabu - zimeujaza usiku.
我也照样经过困苦的日月, 夜间的疲乏为我而定。
4 Hapo nilalapo chini, najiuliza mwenyewe, 'Lini nitatoka kitandani na lini usiku utatoweka?' Nimejawa na kujitupa huku na huko hadi mwanzo wa siku.
我躺卧的时候便说: 我何时起来,黑夜就过去呢? 我尽是反来复去,直到天亮。
5 Mwili wangu umevikwa minyoo na madonda yenye vumbi; maumivu katika ngozi yangu yamekuwa magumu na kisha hutoweka na huendelea tena.
我的肉体以虫子和尘土为衣; 我的皮肤才收了口又重新破裂。
6 Siku zangu zinakimbia kuliko chombo cha kufumia; zinapita bila tumaini.
我的日子比梭更快, 都消耗在无指望之中。
7 Mungu, anakumbuka kwamba maisha yangu ni pumzi tu; jicho langu halitaona mema tena.
求你想念,我的生命不过是一口气; 我的眼睛必不再见福乐。
8 Jicho lake Mungu, huyo anionaye mimi, halitaniangalia tena; Macho ya Mungu yatanitazama, lakini sitakuwako.
观看我的人,他的眼必不再见我; 你的眼目要看我,我却不在了。
9 kama vile wingu liishavyo na kutoweka, hivyo wale waendao sheoli hawatarudi tena kabisa. (Sheol h7585)
云彩消散而过; 照样,人下阴间也不再上来。 (Sheol h7585)
10 Yeye hatarudi tena nyumbani kwake, wala mahali pake hapatamtambua tena.
他不再回自己的家; 故土也不再认识他。
11 Kwa sababu hiyo sitakizuia kinywa changu; Nitasema juu ya maumivu makubwa ya roho yangu; Nitanung'unika juu ya uchungu wa nafsi yangu.
我不禁止我口; 我灵愁苦,要发出言语; 我心苦恼,要吐露哀情。
12 Je mimi ni bahari au kiumbe cha kutisha baharini hata ukaweka mlinzi juu yangu?
我对 神说:我岂是洋海, 岂是大鱼,你竟防守我呢?
13 Hapo nisemapo, 'kitanda changu kitanifariji, na malazi yangu yatatuliza manung'uniko yangu,'
若说:我的床必安慰我, 我的榻必解释我的苦情,
14 halafu unitishapo kwa ndoto na kunitisha kwa maono,
你就用梦惊骇我, 用异象恐吓我,
15 ili nichague kunyongwa na kufa kuliko kulinda mifupa yangu hii.
甚至我宁肯噎死,宁肯死亡, 胜似留我这一身的骨头。
16 Ninayachukia kabisa maisha yangu; sitamani siku zote kuwa hai; usinisumbue maana siku zangu hazifai.
我厌弃性命,不愿永活。 你任凭我吧,因我的日子都是虚空。
17 Je mtu ni nini hata ukatia bidii kwake, na ukaweka akili yako kwake,
人算什么,你竟看他为大, 将他放在心上?
18 na kumwangalia kila asubuhi, na kumjaribu kila mara?
每早鉴察他, 时刻试验他?
19 Je itachukuwa muda gani kabla hujaacha kuniangalia, wala kunisumbua muda wa kutosha kwaajili ya kumeza mate yangu?
你到何时才转眼不看我, 才任凭我咽下唾沫呢?
20 Hata kama nimefanya dhambi, itakusaidia nini, wewe ulindaye wanadamu? Kwa nini umenifanya shabaha yako, kiasi kwamba nimekuwa mzigo kwako?
鉴察人的主啊,我若有罪,于你何妨? 为何以我当你的箭靶子, 使我厌弃自己的性命?
21 Kwa nini hunisamehi makosa yangu na kuniondolea uovu wangu? kwa kuwa sasa nitalala mavumbini; na wewe utanitafuta kwa bidii, lakini sitakuwako.”
为何不赦免我的过犯, 除掉我的罪孽? 我现今要躺卧在尘土中; 你要殷勤地寻找我,我却不在了。

< Ayubu 7 >