< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
respondens autem Iob dixit
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
utinam adpenderentur peccata mea quibus iram merui et calamitas quam patior in statera
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
quasi harena maris haec gravior appareret unde et verba mea dolore sunt plena
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
quia sagittae Domini in me sunt quarum indignatio ebibit spiritum meum et terrores Domini militant contra me
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
numquid rugiet onager cum habuerit herbam aut mugiet bos cum ante praesepe plenum steterit
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
aut poterit comedi insulsum quod non est sale conditum aut potest aliquis gustare quod gustatum adfert mortem
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
quae prius tangere nolebat anima mea nunc prae angustia cibi mei sunt
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
quis det ut veniat petitio mea et quod expecto tribuat mihi Deus
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
et qui coepit ipse me conterat solvat manum suam et succidat me
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
et haec mihi sit consolatio ut adfligens me dolore non parcat nec contradicam sermonibus Sancti
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
quae est enim fortitudo mea ut sustineam aut quis finis meus ut patienter agam
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
nec fortitudo lapidum fortitudo mea nec caro mea aerea est
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
ecce non est auxilium mihi in me et necessarii quoque mei recesserunt a me
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
qui tollit ab amico suo misericordiam timorem Domini derelinquit
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
fratres mei praeterierunt me sicut torrens qui raptim transit in convallibus
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
qui timent pruinam inruet super eos nix
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
tempore quo fuerint dissipati peribunt et ut incaluerit solventur de loco suo
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
involutae sunt semitae gressuum eorum ambulabunt in vacuum et peribunt
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
considerate semitas Theman itinera Saba et expectate paulisper
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
confusi sunt quia speravi venerunt quoque usque ad me et pudore cooperti sunt
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
nunc venistis et modo videntes plagam meam timetis
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
numquid dixi adferte mihi et de substantia vestra donate mihi
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
vel liberate me de manu hostis et de manu robustorum eruite me
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
docete me et ego tacebo et si quid forte ignoravi instruite me
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
quare detraxistis sermonibus veritatis cum e vobis nullus sit qui possit arguere
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
ad increpandum tantum eloquia concinnatis et in ventum verba profertis
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
super pupillum inruitis et subvertere nitimini amicum vestrum
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
verumtamen quod coepistis explete praebete aurem et videte an mentiar
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
respondete obsecro absque contentione et loquentes id quod iustum est iudicate
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
et non invenietis in lingua mea iniquitatem nec in faucibus meis stultitia personabit

< Ayubu 6 >