< Ayubu 6 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Mais Job répondit, et dit:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
Plût à Dieu que mon indignation fût bien pesée, et qu'on mît ensemble dans une balance ma calamité!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Car elle serait plus pesante que le sable de la mer; c'est pourquoi mes paroles sont englouties.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
Parce que les flèches du Tout-puissant sont au dedans de moi; mon esprit en suce le venin; les frayeurs de Dieu se dressent en bataille contre moi.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
L'âne sauvage braira-t-il après l'herbe, et le bœuf mugira-t-il après son fourrage?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Mangera-t-on sans sel ce qui est fade? trouvera-t-on de la saveur dans le blanc d'un œuf?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
Mais pour moi, les choses que je n'aurais pas seulement voulu toucher, sont des saletés qu'il faut que je mange.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
Plût à Dieu que ce que je demande m'arrivât, et que Dieu me donnât ce que j'attends;
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
Et que Dieu voulût m'écraser, et [qu'il voulût] lâcher sa main pour m'achever!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Mais j'ai encore cette consolation, quoique la douleur me consume, et qu'elle ne m'épargne point, que je n'ai point tû les paroles du Saint.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
Quelle est ma force, que je puisse soutenir [de si grands maux]? et quelle [en est] la fin, que je puisse prolonger ma vie?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Ma force est-elle une force de pierre, et ma chair est-elle d'acier?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Ne suis-je pas destitué de secours, et tout appui n'est-il pas éloigné de moi?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
A celui qui se fond [sous l'ardeur des maux, est due] la compassion de son ami; mais il a abandonné la crainte du Tout-puissant.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
Mes frères m'ont manqué comme un torrent, comme le cours impétueux des torrents qui passent;
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Lesquels on ne voit point à cause de la glace, et sur lesquels s'entasse la neige;
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
Lesquels, au temps que la chaleur donne dessus, défaillent; quand ils sentent la chaleur, ils disparaissent de leur lieu;
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
Lesquels serpentant çà et là par les chemins, se réduisent à rien, et se perdent.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
Les troupes des voyageurs de Téma y pensaient, ceux qui vont en Séba s'y attendaient;
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
[Mais] ils sont honteux d'y avoir espéré; ils y sont allés, et ils en ont rougi.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
Certes, vous m'êtes devenus inutiles; vous avez vu ma calamité étonnante, et vous en avez eu horreur.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Est-ce que je vous ai dit: Apportez-moi et me faites des présents de votre bien?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
Et délivrez-moi de la main de l'ennemi, et me rachetez de la main des terribles?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Enseignez-moi, et je me tairai; et faites-moi entendre en quoi j'ai erré.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
Ô combien sont fortes les paroles de vérité! mais votre censure, à quoi tend-elle?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Pensez-vous qu'il ne faille avoir que des paroles pour censurer; et que les discours de celui qui est hors d'espérance, ne soient que du vent?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Vous vous jetez même sur un orphelin, et vous percez votre intime ami.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Mais maintenant je vous prie regardez-moi bien, si je mens en votre présence!
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Revenez, je vous prie, [et] qu'il n'y ait point d'injustice [en vous]; oui, revenez encore; car je ne suis point coupable en cela.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Y a-t-il de l'iniquité en ma langue? et mon palais ne sait-il pas discerner mes calamités?