< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
And he answered Job and he said.
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
Certainly [if] it will be weighed grief my (and destruction my *Q(K)*) in [the] balances people will raise together.
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now more than [the] sand of [the] seas it will be heavy there-fore words my they have been rash.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For [the] arrows of [the] Almighty [are] with me which poison their [is] drinking spirit my [the] terrors of God they are arranged against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
¿ Does it bray a wild donkey on grass or? does it low an ox on fodder its.
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
¿ Is it eaten tasteless [food] because not salt or? [is] there taste in [the] slime of purslane.
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
It refuses to touch [them] self my they [are] like [the] illness of food my.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
Who? will he give it will come petition my and hope my he will give God.
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
And may he be willing God and may he crush me may he loosen hand his and may he cut off me.
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
And may it be still - comfort my and may I jump in anguish [which] not it relents that not I have hidden [the] words of [the] holy [one].
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What? [is] strength my that I will wait and what? [is] end my that I will prolong life my.
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
[the] strength of Stones [is] strength my or? [is] flesh my bronze.
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
¿ If not [is] help my in myself and sound wisdom it has been banished from me.
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
[belongs] to Despairing [person] from friend his loyalty and [the] fear of [the] Almighty he will forsake.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
Brothers my they have acted treacherously like a wadi like a stream-bed of wadis [which] they pass away.
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
That are dark from ice over them it hides itself snow.
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
At [the] time [when] they flow they are silenced in heat its they are dried up from place their.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
They twist [the] paths of way their they go up in the wasteland so they may perish.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
They look [the] caravans of Tema [the] travelers of Sheba they look eagerly for them.
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They are disappointed for he had been confident they come to it and they were disappointed.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For now you have become (it *Q(K)*) you have seen a terror and you were afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
¿ For have I said give for me and from wealth your give a reward for me.
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
And rescue me from [the] hand of an opponent and from [the] hand of ruthless [people] you will ransom me.
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Teach me and I I will keep silent and what? have I erred explain to me.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How! they are painful words of uprightness and what? does it prove completely from you.
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
¿ To reprove words do you plan and to wind [the] words of [one who] despairs.
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Even on a fatherless one you will make fall and you may bargain on friend your.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
And therefore be willing turn on me and on faces your if I will lie.
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Turn back please may not it be injustice (and turn back *Q(K)*) still righteousness my [is] in it.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
¿ [is] there On tongue my injustice or? palate my not does it discern destruction.

< Ayubu 6 >