< Ayubu 6 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then responded Job, and said: —
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
Oh that, weighed, were my vexation, and, my engulfing ruin—into the balances, they would lift up all at once!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For, now, beyond the sand of the seas, would it be heavy, On this account, my words, have wandered.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For, the arrows of the Almighty, are in me, The heat whereof, my spirit is drinking up, The, terrors of GOD, array themselves against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Doth the wild ass bray over grass? Or loweth the ox over his fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Can that which hath no savour be eaten without salt? Or is there any taste in the white of an egg?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
My soul hath refused to touch, Those things, are like disease in my food.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
Oh that my request would come! and, my hope, oh that GOD would grant!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
That it would please GOD to crush me, That he would set free his hand, and cut me off!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
So might it still be my comfort, And I might exult in the anguish he would not spare, —That I had not concealed the sayings of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What is my strength, that I should hope? Or what mine end, that I should prolong my desire?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength, the strength of stones? Or is, my flesh, of bronze?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Is there any help at all in me? Is not, abiding success, driven from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
The despairing, from his friend, should have lovingkindness, or, the reverence of the Almighty, he may forsake.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
Mine own brethren, have proved treacherous like a torrent, like a channel of torrents which disappear:
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Which darken by reason of the cold, over them, is a covering made by the snow:
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
By the time they begin to thaw, they are dried up, as soon as it is warm, they have vanished out of their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
Caravans turn aside by their course, they go up into a waste, and are lost:
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The caravans of Tema looked about, the travelling companies of Sheba, hoped for them:
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They are ashamed that they had trusted, They have come up to one of them, and are confounded.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For, now, ye have come to him, ye see something fearful, and fear.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Is it that I said, Make me a gift, or, out of your abundance, offer a bribe on my behalf;
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
And deliver me from the hand of the adversary? And, out of the hand of tyrants, ransom me?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Show me, and, I, will hold my peace, And, wherein I have erred, cause me to understand.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How pleasant are the sayings that are right! But what can a decision from you, decide?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
To decide words, do ye intend, When, to the wind, are spoken the sayings of one in despair?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Surely, the fatherless, ye would assail, and make merchandise of your friend!
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
But, now, be pleased to turn to me, that it may be, to your faces, if I speak falsehood,
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Reply, I pray you, let there be no perversity, Yea reply even yet, my vindication is in it!
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there, in my tongue, perversity? Or can, my sense, not discern, engulfing ruin?