< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job answered and said:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
O that my grief were weighed thoroughly! That my calamities were put together in the balance!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
Surely they would be heavier than the sand of the sea; On this account were my words rash.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty have pierced me; Their poison drinketh up my spirit; The terrors of God set themselves in array against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Doth the wild ass bray in the midst of grass? Or loweth the ox over his fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Can that which is unsavory be eaten without salt? Is there any taste in the white of an egg?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
That which my soul abhorreth to touch Hath become my loathsome food.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
O that I might have my request, And that God would grant me that which I long for!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
That it would please God to destroy me; That he would let loose his hand, and make an end of me!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
Yet it should still be my consolation, Yea, in unsparing anguish I would exult, That I have not denied the commands of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What is my strength, that I should hope? And what mine end, that I should be patient?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength the strength of stones? Or is my flesh brass?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Alas, there is no help within me! Deliverance is driven from me!
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
To the afflicted, kindness should be shown by a friend; Else he casteth off the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
But my brethren are faithless like a brook; Like streams of the valley that pass away;
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
Which are turbid by reason of the ice, And the snow, which hideth itself in them.
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
As soon as they flow forth, they vanish; When the heat cometh, they are dried up from their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
The caravans turn aside to them on their way; They go up into the desert, and perish.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The caravans of Tema look for them; The companies of Sheba expect to see them;
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They are ashamed that they have relied on them; They come to their place, and are confounded.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
So ye also are nothing; Ye see a terror, and shrink back.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Have I said, Bring me gifts? Or, Give a present for me out of your substance?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
Or, Deliver me from the enemy's hand? Or, Rescue me from the hand of the violent?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Convince me, and I will hold my peace; Cause me to understand wherein I have erred.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How powerful are the words of truth! But what do your reproaches prove?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Do ye mean to censure words? The words of a man in despair are but wind.
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
Truly ye spread a net for the fatherless; Ye dig a pit for your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
Look now upon me, I pray you; For to your very face can I speak falsehood?
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Return, I pray, and let there be no unfairness; Yea, return; —still is my cause righteous.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there iniquity on my tongue? Cannot my taste discern what is sinful?

< Ayubu 6 >