< Ayubu 6 >

1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
And Job answers and says:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
“O that my provocation were thoroughly weighed, And my calamity in balances They would lift up together!
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For now it is heavier than the sands of the sea, Therefore my words have been rash.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For arrows of the Mighty [are] with me, Whose poison is drinking up my spirit. Terrors of God array themselves [for] me!
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Does a wild donkey bray over tender grass? Does an ox low over his provender?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Is an insipid thing eaten without salt? Is there sense in the drivel of dreams?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
My soul is refusing to touch! They [are] as my sickening food.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
O that my request may come, That God may grant my hope!
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
That God would please—and bruise me, Loose His hand and cut me off!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
And yet it is my comfort (And I exult in pain—He does not spare), That I have not hidden The sayings of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What [is] my power that I should hope? And what [is] my end that I should prolong my life?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength the strength of stones? Is my flesh bronze?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Is my help not with me, And substance driven from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
To a despiser of his friends [is] shame, And the fear of the Mighty he forsakes.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
My brothers have deceived as a brook, As a stream of brooks they pass away.
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
That are black because of ice, By them snow hides itself.
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
By the time they are warm they have been cut off, By its being hot they have been Extinguished from their place.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
The paths turn aside of their way, They ascend into emptiness, and are lost.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
Passengers of Tema looked expectingly, Travelers of Sheba hoped for them.
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They were ashamed that one has trusted, They have come to it and are confounded.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
Surely now you have become the same! You see a downfall, and are afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Is it because I said, Give to me? And, By your power bribe for me?
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
And, Deliver me from the hand of an adversary? And, Ransom me from the hand of terrible ones?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Show me, and I keep silent, And what I have erred, let me understand.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How powerful have been upright sayings, And what reproof from you reproves?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
For reproof—do you reckon words? And for wind—sayings of the desperate?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
You cause anger to fall on the fatherless, And are strange to your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
And now, please, look on me, Even to your face do I lie?
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Please turn back, let it not be perverseness, Indeed, turn back again—my righteousness [is] in it.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there perverseness in my tongue? Does my palate not discern calamity?”

< Ayubu 6 >