< Ayubu 6 >
1 Kisha Ayubu akajibu na kusema,
Then Job replied:
2 “Oo, laiti maumivu yangu makubwa yangepimwa; laiti misiba yangu yote mikubwa ingewekwa kwenye mizani!
“If only my grief could be weighed and placed with my calamity on the scales.
3 Kwa kuwa sasa ungekuwa mzito kuliko mchanga wa baharini. Kwa sababu hiyo maneno yangu yamekuwa ya haraka.
For then it would outweigh the sand of the seas— no wonder my words have been rash.
4 Kwa kuwa mishale ya Mwenyezi ipo ndani yangu, moyo wangu umelewa sumu; Vitisho vya Mungu vimejipanga vyenyewe dhidi yangu.
For the arrows of the Almighty have pierced me; my spirit drinks in their poison; the terrors of God are arrayed against me.
5 Je punda mwitu hulia akiwa na malisho? Au ng'ombe huwa dhaifu wakati wa njaa ambapo anachakula?
Does a wild donkey bray over fresh grass, or an ox low over its fodder?
6 Je inawezekana kitu kisicho na ladha kulika bila chumvi? Au kuna radha yoyote katika ute mweupe wa yai?
Is tasteless food eaten without salt, or is there flavor in the white of an egg?
7 Nakataa kuvigusa; kwangu mimi vinafanana na chakula kichukizacho.
My soul refuses to touch them; they are loathsome food to me.
8 Oo, kama nigeweza kupata haja yangu; oo, kama Mungu angeridhia jambo nilitamanilo sana:
If only my request were granted and God would fulfill my hope:
9 kama Mungu ingempendeza kuniangamiza mara moja, kwamba angeulegeza mkono wake na kuyakatilia mbali maisha yangu!
that God would be willing to crush me, to unleash His hand and cut me off!
10 Hii ingeweza kuwa faraja yangu hata sasa - hata kama nafurahia sana maumivu yasiyopungua: kwa kuwa sikuyakana maneno yake Mtakatifu.
It still brings me comfort, and joy through unrelenting pain, that I have not denied the words of the Holy One.
11 Nguvu yangu ni ipi, hata nijaribu kusubiri? Mwisho wangu ni upi, utakao refusha maisha yangu?
What strength do I have, that I should still hope? What is my future, that I should be patient?
12 Je nguvu zangu ni nguvu za mawe? Au mwili wangu umeumbwa kwa shaba nyeusi?
Is my strength like that of stone, or my flesh made of bronze?
13 Je si kweli kwamba sina msaada ndani yangu, na kwamba hekima imeondolewa mbali nami?
Is there any help within me now that success is driven from me?
14 Kwa mtu ambaye yu karibu kuzirai, inapasa uaminifu uonyeshwe na rafiki zake; hata kwake yeye aachaye kumcha Mwenyezi.
A despairing man should have the kindness of his friend, even if he forsakes the fear of the Almighty.
15 Lakini ndugu zangu wamekuwa waaminifu kwangu kama mkondo wa maji jangwani, mfano wa mifereji ya maji ipitayo mpaka pasipo kitu,
But my brothers are as faithless as wadis, as seasonal streams that overflow,
16 ambayo imekuwa mieusi kwa sababu ya barafu juu yake, na kwa sababu ya theluji ambayo hujificha yenyewe ndani yake.
darkened because of the ice and the inflow of melting snow,
17 Wakati zikiyeyuka, hutoweka; kukiwa na joto, hutoweka mahali hapo.
but ceasing in the dry season and vanishing from their channels in the heat.
18 Misafara ambayo husafiri kwa njia yao hugeuka na maji; huzurura jangwani na kisha hupotea.
Caravans turn aside from their routes; they go into the wasteland and perish.
19 Misafara kutoka Tema huitazama, wakati majeshi ya Sheba huitarajia.
The caravans of Tema look for water; the travelers of Sheba hope to find it.
20 Wamevunjika moyo kwa sababu walitumaini kupata maji. Wakaenda huko, lakini walidanganywa.
They are confounded because they had hoped; their arrival brings disappointment.
21 Kwa sasa ninyi rafiki si kitu kwangu; mmeona hali yangu ya kutisha nanyi mwaogopa.
For now you are of no help; you see terror, and you are afraid.
22 Je nilisema kwenu, 'Nipeni kitu furani?' Au, 'nitoleeni zawadi katika mali zenu?'
Have I ever said, ‘Give me something; offer me a bribe from your wealth;
23 Au, 'Niokoeni toka mkononi mwa mtesi wangu?' Au, 'Nitoleeni fidia kwa watesi wangu?'
deliver me from the hand of the enemy; redeem me from the grasp of the ruthless’?
24 Nifundishe, nami nitaishika amani yangu; nifanye nifahamu wapi nilipokosea.
Teach me, and I will be silent. Help me understand how I have erred.
25 Jinsi gani maneno ya kweli yanavyo umiza! Lakini hoja zenu, jee hasa zimenionya nini mimi?
How painful are honest words! But what does your argument prove?
26 Je mnapanga kuyakemea maneno yangu, mnayachukulia maneno ya mtu mwenye kukata tamaa sawa na upepo?
Do you intend to correct my words, and treat as wind my cry of despair?
27 Hasa, mna piga kura kwa ajili ya yatima, na kupatana bei juu ya rafiki yenu kama bidhaa.
You would even cast lots for an orphan and barter away your friend.
28 Sasa, kwa sababu hiyo, tafadhari nitazame, kwa hakika sitasema uongo usoni penu.
But now, please look at me. Would I lie to your face?
29 Rudini, nawasihi; lisiwepo neno la uonevu na nyinyi; Hasa, rudini, sababu zangu ni za haki.
Reconsider; do not be unjust. Reconsider, for my righteousness is at stake.
30 Je mna uovu ulimini mwangu? Je kinywa changu hakiwezi kungundua madhara?
Is there iniquity on my tongue? Can my mouth not discern malice?