< Ayubu 5 >

1 Ita sasa; je kuna yeyote ambaye atakujibu? Utamrudia yupi katika watakatifu hao?
任你呼求,看有誰答應你﹖諸聖者中,看你轉向那一位﹖
2 Kwa kuwa hasira huua mtu mpumbavu; wivu huua mjinga.
的確,憂憤殺死愚人,怒火使痴者喪生。
3 Nimemuona mtu mpumbavu akishika mzizi, lakini ghafla niliyalaani makazi yake.
我知道:愚人一根深蒂固,他的居所即被詛咒;
4 Watoto wake wako mbali na uzima; wameangamia langoni mwa mji. Hakuna yeyote atakaye waponya.
他的子女,無人支援,在城門前被踐踏,無人救護。
5 Mwenye njaa hula mavuno yao; hata huyachukua katikati ya miiba. Wenye kiu huzihemea mali zao.
他們收穫的,飢餓者來吃;且將剩餘的,搶去儲存;他們的財富,為口渴者喝盡。
6 Kwa kuwa magumu hayatoki udongoni; wala taabu haichipuki katika nchi.
因為災禍不是由土中而來,憂患不是生自地中;
7 Badala yake, wanadamu huzaliwa kwaajili ya taabu, kama tu cheche za moto zirukavyo juu.
而是人自尋苦惱,如雛鷹自會飛翔。
8 Lakini kwa mimi, ningemrudia Mungu mwenyewe; kwake ningeaminisha kusudi langu -
如果是我,我必投奔天主,向天主陳訴我的案情。
9 yeye afanyae makuu na mambo yasiyochunguzika, mambo ya ajabu yasiyo na hesabu.
他所作的大事,高深莫測;他所行的奇事,不可勝數:
10 Hutoa mvua juu ya nchi, na huyapeleka maji mashambani.
他使雨落在地上,引水滋潤郊田;
11 Hufanya haya kwaajili ya kuwainua juu hao walio chini; huwapandisha sehemu salama hao waombolezao.
使卑微的人高昇,使受苦的人獲得救助;
12 Yeye huharibu mipango ya watu wenye hila, ili mikono yao isipate mafanikio.
粉碎狡猾人的計謀,使他們的作為一無所成;
13 Yeye huwanasa watu wenye hekima katika matendo ya hila zao wenyewe; mipango ya watu waliogeuzwa huharibika haraka.
以智者的計謀捕捉智者,使奸猾人的策畫即時成空;
14 Wao hupatwa na giza wakati wa mchana, na hupapasa mchana kama vile ni usiku.
他們白日遇到黑暗,正午摸索如在夜間;
15 Lakini yeye huokoa maskini kwa upanga wa vinywa vyao na mhitaji kwa mkono wa mtu mwenye nguvu.
他搭救被剝削者脫離人口,挽救窮人擺脫強暴的手。
16 Hivyo mtu maskini ana matumaini, na udhalimu hufumba kinywa chake mwenyewe.
如此,貧苦的人獲得希望,邪惡將閉口無言。
17 Tazama, amebarikiwa mtu ambaye hutiwa adabu na Mungu; kwa sababu hiyo, usidharau uongozi wa Mwenyezi.
的確,天主所懲戒的人是有福的:全能者的訓戒,你不可忽視。
18 Kwa kuwa yeye hujeruhi na kisha huuguza; yeye hutia jeraha na kisha mikono yake huponya.
因為他打傷了,而又包紮傷口;他擊碎了,而又親手治療。
19 Yeye atakuokoa na mateso sita; kweli, katika mateso saba, hakuna uovu utakao kugusa.
你六次遭難,他次次拯救;到第七次,災難不會臨於你。
20 Wakati wa njaa atakukomboa na kifo, na kwa uwezo wa upanga wakati wa vita.
饑饉中,他必救你不死;戰爭中,必使你得免刀劍。
21 Wewe utafichwa na mateso ya ulimi; na usitishike na uharibifu utakapokuja.
唇槍舌劍,你必能躲藏;大難來臨,你不必張惶;
22 Wewe utaufurahia uharibifu na njaa, na hutatishika na wanyama wakali wa nchi.
對大難和饑荒,你可置之一笑;對地上的野獸,也不用驚惶。
23 Kwa kuwa wewe utakuwa na mapatano na mawe ya shambani mwako, na wanyama wa mwituni watakuwa na amani na wewe.
你將與田野的頑石立約,曠野的猛獸必與你和好。
24 Wewe utajua kwamba hema lako lina usalama; utatembelea zizi la kondoo wako na hutakosa kitu chochote.
你將見到你的帳幕平安無恙,察看羊欄時,一無所失。
25 Pia utafahamu kwamba uzao wako utakuwa mwingi, na vizazi vyako vitakuwa kama nyasi ardhini.
你將確知子孫繁昌,你的苗裔猶如田野青草。
26 Wewe utafika kaburini kwako mwenye umri kamili, kama vile rundo la mashuke ya nafaka liendavyo juu wakati wake.
你必高年纔葬於墓,好像麥梱準時收藏。
27 Tazama, tumelipeleleza jambo hili; ndivyo lilivyo; lisikie, na ulifahamu kwa ajili yako mwenyewe.”
看,這是我們所觀察的真理,你若細聽,自會獲益良多。

< Ayubu 5 >