< Ayubu 42 >
1 Kisha Ayubu akamjibu Yahweh na kusema,
Then Job replied to Yahweh. [He said],
2 “Ninajua kwamba unaweza kufanya mambo yote, ya kuwa hakuna kusudi lako linaweza kuzuiliwa.
“I know that you can do everything and that no one can stop you from doing what you want to do.
3 Ni nani huyo ambaye pasipo maarifa huificha mipango? Kwa kweli nilisema mambo ambayo sikuyaelewa, mambo magumu kwangu kuyafahamu, ambayo juu yake sikujua chochote.
[You asked me], ‘(Who are you, who by speaking ignorantly, question what I plan to do?/You have no right to question what I plan to do by speaking ignorantly.)’ [RHQ] It is true that I spoke about things that I did not understand, things that are very wonderful/marvelous, and therefore I am not able to know them.
4 Uliniambia, 'Sikiliza sasa, nami nitasema; nitakuuliza mambo, nawe utaniambia.'
You said to me, ‘Listen while I talk to you. I want to ask you some questions, so prepare yourself to answer them.’
5 Nimekuwa nikikusikia kwa usikivu wa sikio langu, lakini sasa jicho langu linakuona wewe.
I had heard about you previously, but now [it is as though] I have seen you with my own eyes.
6 Basi ninajidharau mwenyewe; ninatubu kwa mavumbi na majivu.”
Therefore I (am ashamed of/withdraw) what I said, and I sit in dust and ashes to show that I am sorry [for what I said].”
7 Ilitokea baada ya kuwa amekwisha kusema maneno hata kwa Ayubu, Yahweh alimwambia Elifazi Mtemani, “Ghadhabu yangu imewaka dhidi yako na dhidi ya marafiki zako wawili kwa kuwa hamkusema maneno ya haki juu yangu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.
After Yahweh said these things to Job, he said to Eliphaz, “I am angry with you and your two friends, [Bildad and Zophar], because what my servant Job said about me was right/true, but what you have spoken about me was not right/true.
8 Sasa basi, jitwalieni mafahari saba na mabeberu saba, kisha mmwendee mtumishi wangu Ayubu na mtoe sadaka ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Ndipo Mtumishi wangu Ayubu atawaombea ninyi, nami nitayapokea maombi yake, ili kwamba nisiwashughulikie sawasawa na upumbavu wenu. Maana hamkusema mambo ya haki juu yangu, kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”
So now you must take to Job seven young bulls and seven rams and [kill them and] burn them on the altar as a sacrifice for yourselves. Then Job will pray for you, and I will do what he requests me to do, [and I will forgive you for speaking wrongly about me]. I will not punish you, even though you deserve to be punished, because what you said about me was not right/true, but what Job said about me was right/true.”
9 Basi Elifazi Mtemani, Bildadi Mshuhi na Zofari Mnaamathi walienda na kufanya kama vile Yahweh alivyowaamuru, na Mungu alimtakabali Ayubu.
So Eliphaz, Bildad, and Zophar did what Yahweh commanded them to do, and Yahweh did what Job requested him to do [for the three of them].
10 Na wakati Ayubu alimpowaombea rafiki zake, Yahweh alirejeza bahati yake. Yahweh alimjalia mara mbili ya kile alichokimiliki hapo awali.
After Job prayed for his three friends, Yahweh [healed him and] caused him to become rich again. Yahweh gave him twice as many things as he had before.
11 Ndipo ndugu zake na Ayubu, na wale jamaa zake wote walikuwa wanajuana naye hapo mwanzo, walikuja hapo kwake na kula chakula pamoja naye katika nyumba yake. Waliomboleza pamoja naye na walimfariji kwa ajili majanga yote ambayo Yahweh alikuwa ameyaleta juu yake. Kila mtu alimpa Ayubu kipande cha fedha na pete ya dhahabu.
Then all his brothers and sisters, and all the people who had known him before, came to his house, and they ate a meal together. They consoled/comforted [DOU] him because of all the troubles that Yahweh had allowed him to experience.
12 Yahweh aliubarikiwa mwisho wa maisha ya Ayubu kuliko mwanzo wake; alikuwa na kondoo kumi na nne elfu, ngamia elfu sita, jozi elfu moja, na punda jike elfu moja.
Then Yahweh blessed Job in the second half of his life more than he had blessed him in the first half of his life. He now acquired/owned 14,000 sheep, 6,000 camels, 2,000 oxen, and 1,000 female donkeys.
13 Pia alikuwa na wana saba na mabinti watatu.
And he also had seven [more] sons and three [more] daughters.
14 Binti wa kwanza alimwita Yemima, na wa pili Kezia, na wa tatu Kerenihapuki.
He named the first daughter Jemimah, he named the second daughter Keziah, and he named the third daughter Keren-Happuch.
15 Katika nchi yote hawakupatikana wanawake wazuri kama mabinti wa Ayubu. Baba yao aliwapa urithi miongoni mwa kaka zao.
In all of [Uz] land there were no young women who were as beautiful as the daughters of Job, and Job declared that they would inherit some of his possessions, just like their brothers would inherit some.
16 Baada ya haya, Ayubu aliishi miaka 140; aliwaona wana wake na wana wa wanawe, hata kizazi cha nne.
After that, Job lived 140 more years. Before he died, he (saw/enjoyed being with) his great-great-grandchildren.
17 Basi Ayubu alifariki, akiwa mzee na akijawa na siku nyingi.
He was very old [DOU] when he died.