< Ayubu 41 >
1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
¿Puedes tú sacar con un anzuelo el cocodrilo, atar con una cuerda su lengua?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
¿Pondrás una soga en su nariz, y perforarás con garfio su quijada?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
¿Se acercará a ti con palabras sumisas o te hablará con lisonjas?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
¿Hará un pacto contigo para que lo tomes como esclavo perpetuo?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
¿Jugarás con él como con un pájaro? ¿Lo atarás para entretener a tus niñas?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
¿Los comerciantes harán negocio por él? ¿Lo cortarán en trozos entre los mercaderes?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
¿Podrás abrirle el cuero con lancetas, o su cabeza con arpones?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Pon tu mano sobre él. Recuerda la batalla con él. No lo volverás a hacer.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Ciertamente la esperanza de esta pelea queda frustrada. Un hombre desfallece con solo verlo.
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Nadie se atreve a despertarlo. ¿Entonces quién puede estar en pie delante de Mí?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
¿Quién me dio primero a Mí, para que Yo le restituya? Todo lo que hay debajo del cielo es mío.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
No guardaré silencio acerca de sus miembros, ni de su gran fuerza ni de su excelente figura.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
¿Quién levanta la primera capa de su envoltura y penetra a través de su doble coraza?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
¿Quién abre la parte posterior de su boca rodeada de dientes espantosos?
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Sus fuertes escamas son su orgullo, cerradas entre sí como firme sello,
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
tan unidas la una con la otra que ni el aire pasa entre ellas.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Están soldadas, cada una a su vecina, trabadas entre sí, no se pueden separar.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Su estornudo lanza destellos de luz. Sus ojos son como los párpados de la aurora.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
De la parte posterior de su boca salen llamaradas y se escapan centellas de fuego.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
De sus fosas nasales sale vapor como el de una olla que hierve al fuego.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Su aliento enciende los carbones. Salen llamaradas de las partes posteriores de su boca.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
En su nuca se asienta la fuerza. Ante él cunde el terror.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Los pliegues de su carne son compactos. Están firmes en él y no se mueven.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Su corazón es duro como la piedra, como la piedra inferior de un molino.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Cuando se levanta, tiemblan los valientes, y por el quebrantamiento, retroceden.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
La espada no lo alcanza, ni la lanza, ni la lanceta, ni la flecha, ni la lanza arrojadiza.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Para él el hierro es como pasto, y el bronce, madera carcomida.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
No lo ahuyentan las flechas. Las piedras de la honda le son como rastrojo.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Los garrotes le son como hojarasca. Se burla del brillo del arma arrojadiza.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Por debajo tiene conchas puntiagudas, se extiende como un trillo sobre el lodo.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Hace lo profundo del mar hervir como una olla. Lo convierte como una olla de ungüento.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Detrás de él brilla una estela de agua como barba encanecida.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Nada hay semejante a él sobre la tierra. Fue hecho exento de temor.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Menosprecia todo lo elevado. Es rey de todos los hijos del orgullo.