< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
an extrahere poteris Leviathan hamo et fune ligabis linguam eius
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
numquid pones circulum in naribus eius et armilla perforabis maxillam eius
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
numquid multiplicabit ad te preces aut loquetur tibi mollia
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
numquid feriet tecum pactum et accipies eum servum sempiternum
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
numquid inludes ei quasi avi aut ligabis illum ancillis tuis
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
concident eum amici divident illum negotiatores
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
numquid implebis sagenas pelle eius et gurgustium piscium capite illius
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
pone super eum manum tuam memento belli nec ultra addas loqui
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
ecce spes eius frustrabitur eum et videntibus cunctis praecipitabitur
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
non quasi crudelis suscitabo eum quis enim resistere potest vultui meo
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
quis ante dedit mihi ut reddam ei omnia quae sub caelo sunt mea sunt
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
non parcam ei et verbis potentibus et ad deprecandum conpositis
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
quis revelavit faciem indumenti eius et in medium oris eius quis intrabit
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
portas vultus eius quis aperiet per gyrum dentium eius formido
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
corpus illius quasi scuta fusilia et conpactum squamis se prementibus
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
una uni coniungitur et ne spiraculum quidem incedit per eas
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
una alteri adherebunt et tenentes se nequaquam separabuntur
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
sternutatio eius splendor ignis et oculi eius ut palpebrae diluculi
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
de ore eius lampades procedunt sicut taedae ignis accensae
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
de naribus eius procedit fumus sicut ollae succensae atque ferventis
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
halitus eius prunas ardere facit et flamma de ore eius egreditur
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
in collo eius morabitur fortitudo et faciem eius praecedet egestas
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
membra carnium eius coherentia sibi mittet contra eum fulmina et ad locum alium non ferentur
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
cor eius indurabitur quasi lapis et stringetur quasi malleatoris incus
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
cum sublatus fuerit timebunt angeli et territi purgabuntur
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
cum adprehenderit eum gladius subsistere non poterit neque hasta neque torax
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
reputabit enim quasi paleas ferrum et quasi lignum putridum aes
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
non fugabit eum vir sagittarius in stipulam versi sunt ei lapides fundae
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
quasi stipulam aestimabit malleum et deridebit vibrantem hastam
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
sub ipso erunt radii solis sternet sibi aurum quasi lutum
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
fervescere faciet quasi ollam profundum mare ponet quasi cum unguenta bulliunt
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
post eum lucebit semita aestimabit abyssum quasi senescentem
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
non est super terram potestas quae conparetur ei qui factus est ut nullum timeret
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
omne sublime videt ipse est rex super universos filios superbiae

< Ayubu 41 >