< Ayubu 41 >
1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Ziehst du das Krokodil mit der Angel heraus, legst du ihm einen Zaum ins Maul?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Kannst du einen Ring an seine Nase legen und einen Haken durch seine Kinnbacken stoßen?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Wird es dich lange bitten oder dir Zärtlichkeiten sagen?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Wird es einen Bund mit dir schließen, daß du es zum ewigen Knechte machest?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Kannst du mit ihm spielen wie mit einem Vögelein, oder es anbinden für deine Mädchen?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Verkaufen es die Genossen untereinander, oder teilen es die Händler unter sich?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Kannst du seine Haut mit Pfeilen spicken und mit Fischerhaken seinen Kopf?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Lege deine Hand daran. Du wirst des Kampfes nicht vergessen, wirst es nicht zum zweitenmal tun!
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Siehe, die Hoffnung auf dasselbe wird getäuscht; fällt man nicht schon bei seinem Anblick dahin?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Niemand ist so kühn, daß er es reizen möchte; wer kann aber vor Mir bestehen?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Wer ist mir zuvorgekommen, daß ich es ihm vergelte? Unter dem ganzen Himmel ist alles mein!
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Ich will von seinen Gliedern nicht schweigen, sondern reden von seiner großen und schönen Gestalt.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Wer entblößt es von seinem Schuppenpanzer und greift ihm in sein doppeltes Gebiß?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Wer öffnet die Türen seines Rachens? Seine Zähne verbreiten Schrecken.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Prächtig sind seine starken Schilder, fest zusammengeschlossen und versiegelt;
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
einer fügt sich an den andern, daß kein Luftzug dazwischen kommt;
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
sie hängen fest zusammen, sind geschlossen und trennen sich nicht.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Sein Niesen strahlt wie Licht, und seine Augen sind wie die Wimpern der Morgenröte.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Aus seinem Rachen schießen Fackeln, Feuerfunken entsprühen ihm.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Dampf geht auf von seinen Nüstern, und der Sumpf wird wie ein siedender Topf.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Sein Atem facht Kohlen an, eine Flamme schießt aus seinem Munde.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Stärke wohnt auf seinem Nacken und Schrecken zieht vor ihm her.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Die Wampen seines Fleisches sitzen fest wie angegossen und bewegen sich nicht.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Sein Herz ist hart wie Stein und so fest wie der untere Mühlstein.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Die Helden erbeben, wenn es auffährt; vor Zittern geht ihr Bogen fehl.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Greift man es mit dem Schwerte an, so haftet dieses nicht, kein Speer, kein Wurfspieß und kein Pfeil.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Es achtet Eisen für einen Strohhalm, und Erz für faules Holz.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
Kein Pfeil vermag es in die Flucht zu schlagen, und Schleudersteine fallen wie Spreu von ihm ab.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Es achtet die Keule für einen Halm und verlacht das Sausen der Spieße.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Unter ihm sind spitze Scherben, es zieht wie ein Dreschschlitten über den Schlamm dahin.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Es macht die Tiefe sieden wie einen Kessel, macht das Meer zu einem Salbentopf.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Hinter ihm her leuchtet der Pfad, es macht die Flut den Silberhaaren gleich.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Auf Erden ist nicht seinesgleichen; es ist gemacht, um ohne Furcht zu sein.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Es schaut alle Hohen [furchtlos] an, es ist ein König über alle Stolzen.