< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Pourras-tu enlever Léviathan à l’hameçon, et avec une corde lier sa langue?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Est-ce que tu mettras un cercle dans ses narines, ou avec un anneau perceras-tu sa mâchoire?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Est-ce qu’il t’adressera de nombreuses prières, ou te dira-t-il de douces paroles?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Est-ce qu’il fera avec toi un pacte, et le recevras-tu comme un esclave éternel?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Est-ce que tu te joueras de lui comme d’un oiseau, ou le lieras-tu pour tes servantes?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Des amis le découperont-ils, ou des marchands le partageront-ils?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Est-ce que tu rempliras de sa peau des filets, et un réservoir de poissons de sa tête?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Mets sur lui ta main: souviens-toi de la guerre, et ne continue pas à parler.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Voilà que son espoir le trompera, et à la vue de tous il se précipitera
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Je ne suis pas assez cruel pour le susciter: car qui peut résister à mon visage;
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Qui m’a donné le premier, afin que je lui rende? Tout ce qui est sous le ciel est à moi.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Je ne l’épargnerai pas, malgré ses discours arrogants et ses paroles suppliantes.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Qui découvrira la face de son vêtement? Et qui entrera dans le milieu de sa gueule?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Les portes de son visage, qui les ouvrira? autour de ses dents habite la terreur.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Son corps est comme des boucliers jetés en fonte et couvert d’écaillés épaisses et serrées.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
L’une est jointe à l’autre, et pas même l’air ne passe entre elles.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
L’une s’attache à l’autre, et se tenant, jamais elles ne se sépareront.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Son éternument, c’est l’éclat du feu, et ses yeux sont comme les paupières de l’aurore.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
De sa gueule sortent des lampes, comme des torches allumées.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
De ses narines sort une fumée comme celle d’un pot mis au feu et bouillant.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Son souffle fait brûler des charbons, et une flamme sort de sa bouche.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Dans son cou résidera sa force, et devant sa face marche la famine.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Les parties de ses chairs adhèrent entre elles: Dieu lancera des foudres contre lui, et elles ne se porteront vers aucun autre lieu.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Son cœur se durcira comme une pierre, et il se resserrera comme une enclume de marteleur.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Lorsqu’il s’élèvera, des anges craindront, et, épouvantés, ils se purifieront.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Lorsque le glaive l’atteindra, ni lance, ni cuirasse ne pourra subsister.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Car il regardera le fer comme de la paille, et l’airain comme un bois pourri.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
L’archer ne le mettra pas en fuite, les pierres de la fronde sont devenues pour lui une paille légère.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Il estimera le marteau comme une paille légère, et il se rira de celui qui brandira la lance.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sous lui seront les rayons du soleil, et il fera son lit sur l’or comme sur la boue.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Il fera bouillir comme un pot la profonde mer, et il la rendra comme des essences lorsqu’elles sont en ébullition.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Derrière lui un sentier répandra la lumière, et l’abîme paraîtra comme un vieillard aux blancs cheveux.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Il n’est pas sur la terre de puissance qui puisse être comparée à lui, qui a été fait pour ne craindre personne.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Il voit tout ce qu’il y a d’élevé au-dessous de lui; c’est lui qui est le roi de tous les fils de l’orgueil.

< Ayubu 41 >