< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Enlèveras-tu le Léviathan avec l'hameçon, et le tireras-tu par sa langue avec le cordeau [de l'hameçon] que tu auras jeté dans l'eau?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Mettras-tu un jonc dans son nez? ou perceras-tu ses mâchoires avec une épine?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Emploiera-t-il auprès de toi beaucoup de prières? ou te parlera-t-il doucement?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Fera-t-il un accord avec toi, et le prendras-tu pour esclave à toujours?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
T'en joueras-tu comme d'un petit oiseau? et l'attacheras-tu pour tes jeunes filles?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Des amis se régaleront-ils de sa chair? sera-t-il partagé entre les marchands?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Rempliras-tu sa peau de pointes? et sa tête [entrerait-elle] dans une nasse de poissons?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Mets ta main sur lui; il ne te souviendra jamais de lui faire la guerre.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Voilà, l'espérance qu'on avait de le prendre est frustrée; [et] ne sera-t-on pas même atterré par son regard?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
Il n'y a point d'homme assez courageux pour le réveiller; qui est-ce donc qui se présentera devant moi?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Qui est-ce qui m'a prévenu, et je [le] lui rendrai? Ce qui est sous tous les cieux est à moi.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
Je ne me tairai point de ses membres, ni de ce qui concerne ses forces, ni de la grâce de l'arrangement [des parties de son corps].
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Qui est-ce qui découvrira le dessus de sa couverture, et se jettera entre les deux branches de son mors?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Qui est-ce qui ouvrira les portes de sa gueule? La terreur se tient autour de ses dents.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
Les lames de ses boucliers ne sont que magnificence; elles sont étroitement serrées [comme] avec un cachet.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
L'une approche de l'autre, et le vent n'entre point entre-deux.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
Elles sont jointes l'une à l'autre, elles s'entretiennent, et ne se séparent point.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
Ses éternuements éclaireraient la lumière, et ses yeux sont [comme] les paupières de l'aube du jour.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Des flambeaux sortent de sa bouche, et il en rejaillit des étincelles de feu.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Une fumée sort de ses narines comme d'un pot bouillant, ou d'une chaudière.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
Son souffle enflammerait des charbons, et une flamme sort de sa gueule.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
La force est dans son cou, et la terreur marche devant lui.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
Sa chair est ferme, tout est massif en lui, rien n'y branle.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
Son cœur est dur comme une pierre, même comme une pièce de la meule de dessous.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
Les plus forts tremblent quand il s'élève, et ils ne savent où ils en sont, voyant comme il rompt tout.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
Qui s'en approchera avec l'épée? ni elle, ni la lance, ni le dard, ni la cuirasse, ne pourront point subsister [devant lui].
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
Il ne tient pas plus de compte du fer que de la paille; et de l'airain, que du bois pourri.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
La flèche ne le fera point fuir, les pierres d'une fronde lui sont comme du chaume.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Il tient les machines de guerre comme des brins de chaume; et il se moque du javelot qu'on lance sur lui.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Il a sous soi des tests aigus, et il abat [sous soi] des roseaux pointus [en se couchant] sur la boue.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
Il fait bouillonner le gouffre comme une chaudière, et rend semblable la mer à un chaudron de parfumeur.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Il fait reluire après soi son sentier, et on prendrait l'abîme pour une tête blanchie de vieillesse.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Il n'y a rien sur la terre qui lui puisse être comparé, ayant été fait pour ne rien craindre.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
Il voit [au-dessous de lui] tout ce qu'il y a de plus élevé; il est Roi sur tous les plus fiers animaux.

< Ayubu 41 >