< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Canst thou draw forth the crocodile with a hook, Or press down his tongue with a cord?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Canst thou put a rope into his nose, Or pierce his cheek with a hook?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he make many entreaties to thee? Will he speak soft words to thee?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Will he make a covenant with thee? Canst thou take him for a servant for ever?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Canst thou play with him, as with a bird? Or canst thou bind him for thy maidens?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Do men in company lay snares for him? Do they divide him among the merchants?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Canst thou fill his skirt with barbed irons, Or his head with fish-spears?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Do but lay thy hand upon him, —Thou wilt no more think of battle!
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Behold, his hope is vain! Is he not cast down at the very sight of him?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None is so fierce that he dare stir him up; Who then is he that can stand before me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who hath done me a favor, that I must repay him? Whatever is under the whole heaven is mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I will not be silent concerning his limbs, And his strength, and the beauty of his armor.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who can uncover the surface of his garment? Who will approach his jaws?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who will open the doors of his face? The rows of his teeth are terrible!
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
His glory is his strong shields, United with each other, as with a close seal.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
They are joined one to another, So that no air can come between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They cleave fast to each other, They hold together, and cannot be separated.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezing sendeth forth light, And his eyes are like the eyelashes of the morning.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Out of his mouth go flames, And sparks of fire leap forth.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
From his nostrils issueth smoke, as from a heated pot, or caldron.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath kindleth coals, And flames issue from his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
In his neck dwelleth strength, And terror danceth before him.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flakes of his flesh cleave fast together; They are firm upon him, and cannot be moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart is solid like a stone; Yea, solid like the nether millstone.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
When he riseth up, the mighty are afraid; Yea, they lose themselves for terror.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
The sword of him that assaileth him doth not stand, The spear, the dart, nor the habergeon.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He regardeth iron as straw, And brass as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The arrow cannot make him flee; Sling-stones to him become stubble;
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Clubs are accounted by him as straw; He laugheth at the shaking of the spear.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Under him are sharp potsherds; He spreadeth out a thrashing-sledge upon the mire.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He maketh the deep to boil like a caldron; He maketh the sea like a pot of ointment.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
Behind him he leaveth a shining path; One would think the deep to be hoary.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
Upon the earth there is not his master; He is made without fear.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He looketh down upon all that is high; He is king over all the sons of pride.

< Ayubu 41 >