< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
“Do you draw leviathan with a hook? And do you let down his tongue with a rope?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Do you put a reed in his nose? And pierce his jaw with a thorn?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Does he multiply supplications to you? Does he speak tender things to you?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Does he make a covenant with you? Do you take him for a perpetual servant?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Do you play with him as a bird? And do you bind him for your girls?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
(Companions feast on him, They divide him among the merchants!)
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Do you fill his skin with barbed irons? And his head with fish-spears?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Place your hand on him, Remember the battle—do not add!
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Behold, the hope of him is found a liar, Also, is one not cast down at his appearance?
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
None so fierce that he awakes him, And who [is] he [who] stations himself before Me?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who has brought before Me and I repay? Under the whole heavens it [is] Mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I do not keep silent concerning his parts, And the matter of might, And the grace of his arrangement.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who has uncovered the face of his clothing? Who enters within his double bridle?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who has opened the doors of his face? Around his teeth [are] terrible.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
A pride—strong ones of shields, Shut up—a close seal.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
They draw near to one another, And air does not enter between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They adhere to one another, They stick together and are not separated.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezings cause light to shine, And his eyes [are] as the eyelids of the dawn.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Flames go out of his mouth, sparks of fire escape.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Smoke goes forth out of his nostrils, As a blown pot and reeds.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath sets coals on fire, And a flame goes forth from his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Strength lodges in his neck, And grief exults before him.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The flakes of his flesh have adhered—Firm on him—it is not moved.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart [is] firm as a stone, Indeed, firm as the lower piece.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
The mighty are afraid at his rising, From his breakings they keep themselves free.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
The sword of his overtaker does not stand, Spear, dart, and breastplate.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
He reckons iron as straw, bronze as rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The son of the bow does not cause him to flee, Stones of the sling are turned into stubble by him.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
Darts have been reckoned as stubble, And he laughs at the shaking of a javelin.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
Sharp points of clay [are] under him, He spreads gold on the mire.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He causes the deep to boil as a pot, He makes the sea as a pot of ointment.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
He causes a path to shine after him, One thinks the deep to be hoary.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
There is not on the earth his like, That is made without terror.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He sees every high thing, He [is] king over all sons of pride.”

< Ayubu 41 >