< Ayubu 41 >

1 Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
Can you draw out the leviathan with a hook, and can you bind his tongue with a cord?
2 Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
Can you place a ring in his nose, or bore through his jaw with an arm band?
3 Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
Will he offer many prayers to you, or speak to you quietly?
4 Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
Will he form a covenant with you, and will you accept him as a servant forever?
5 Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
Will you play with him as with a bird, or tether him for your handmaids?
6 Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
Will your friends cut him into pieces, will dealers distribute him?
7 Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
Will you fill up bags with his hide, and let his head be used as a home for fishes?
8 Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
Place your hand upon him; remember the battle and speak no more.
9 Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
Behold, his hope will fail him, and in the sight of all, he will be thrown down.
10 Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
I will not rouse him, as the cruel would do, for who is able to withstand my countenance?
11 Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
Who has given to me beforehand, so that I should repay him? All things that are under heaven are mine.
12 Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
I will not spare him, nor his powerful words and counterfeit attempts at supplication.
13 Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
Who can reveal the beauty of his garment? And who can enter the middle of his mouth?
14 Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
Who can open the doors of his face? I gave fear to the circle of his teeth.
15 Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
His body is like shields fused together, like dense scales pressed over one another.
16 Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
One is joined to another, and not even air can pass between them.
17 Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
They adhere to one another, and they hold themselves in place and will not be separated.
18 Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
His sneezing has the brilliance of fire, and his eyes are like the eyelids of the morning.
19 Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
Lamps proceed from his mouth, like torches of fire burning brightly.
20 Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
Smoke passes out of his nostrils, like a pot that is heated and boiling.
21 Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
His breath causes coal to burn, and a flame comes forth from his mouth.
22 Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
Strength dwells in his neck, and destitution goes before his presence.
23 Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
The parts of his body work in harmony together. He will send lightning bolts against him, and they will not be carried to another place.
24 Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
His heart will be as hard as a stone and as dense as a blacksmith’s anvil.
25 Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
When he will be raised up, the angels will be afraid, and, because they are terrified, they will purify themselves.
26 Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
When a sword catches up with him, it will not be able to settle in, nor a spear, nor a breastplate.
27 Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
For he will consider iron as if it were chaff, and brass as if it were rotten wood.
28 Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
The archer will not cause him to flee; the stones of the sling have been turned into stubble for him.
29 Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
He will treat the hammer as if it were stubble, and he will ridicule those who brandish the spear.
30 Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
The beams of the sun will be under him, and he will dispense gold to them as if it were clay.
31 Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
He will make the depths of the sea boil like a pot, and he will set it to bubble just as ointments do.
32 Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
A path will shine after him; he will esteem the abyss as if it were weakening with age.
33 Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
There is no power on the earth that is being compared to him, who has been made so that he fears no one.
34 Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”
He sees every prominent thing; he is king over all the sons of arrogance.

< Ayubu 41 >