< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
et adiecit Dominus et locutus est ad Iob
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
numquid qui contendit cum Deo tam facile conquiescit utique qui arguit Deum debet respondere ei
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
respondens autem Iob Domino dixit
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
qui leviter locutus sum respondere quid possum manum meam ponam super os meum
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
unum locutus sum quod utinam non dixissem et alterum quibus ultra non addam
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
respondens autem Dominus Iob de turbine ait
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
accinge sicut vir lumbos tuos interrogabo te et indica mihi
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
numquid irritum facies iudicium meum et condemnabis me ut tu iustificeris
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
et si habes brachium sicut Deus et si voce simili tonas
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
circumda tibi decorem et in sublime erigere et esto gloriosus et speciosis induere vestibus
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
disperge superbos furore tuo et respiciens omnem arrogantem humilia
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
respice cunctos superbos et confunde eos et contere impios in loco suo
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
absconde eos in pulvere simul et facies eorum demerge in foveam
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
et ego confitebor quod salvare te possit dextera tua
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
ecce Behemoth quem feci tecum faenum quasi bos comedet
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
fortitudo eius in lumbis eius et virtus illius in umbilicis ventris eius
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
constringit caudam suam quasi cedrum nervi testiculorum eius perplexi sunt
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
ossa eius velut fistulae aeris cartilago illius quasi lamminae ferreae
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
ipse principium est viarum Dei qui fecit eum adplicabit gladium eius
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
huic montes herbas ferunt omnes bestiae agri ludent ibi
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
sub umbra dormit in secreto calami et locis humentibus
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
protegunt umbrae umbram eius circumdabunt eum salices torrentis
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
ecce absorbebit fluvium et non mirabitur habet fiduciam quod influat Iordanis in os eius
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
in oculis eius quasi hamo capiet eum et in sudibus perforabit nares eius

< Ayubu 40 >