< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
Then Yahweh said to Job,
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
“Do you still want to argue with me, the Almighty One? Since you criticize me, (you should be able to answer my questions!/why are you not able to answer my questions?) [RHQ]”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Then Job replied to Yahweh,
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
“[Now I realize that] I am completely worthless. So (how could I answer [those questions]?/I could not possibly answer [those questions]!) [RHQ] I will put my hand over my mouth [and not say anything].
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
I have already said more than I should have said, so now I will say nothing more.”
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
Then Yahweh [again] spoke to Job from inside the great windstorm. He said,
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
“I want to ask you some [more] questions. So as men prepare themselves for a difficult task [MET], prepare yourself again to answer some [more] questions.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
“Are you going to accuse me and say that I am unjust? Are you going to say that what I have done is wrong, in order that you can say that what you have done is right?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Are you as powerful [MTY] as I am? Can your voice sound [as loud] as thunder, as mine can?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
[If you can do that], put on the robes that show that you are glorious and are greatly honored!
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Show that you are very angry; show that you have the right/authority to humble people who are [very] proud!
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Humble those proud people [just] by looking at them [angrily] Crush wicked people quickly!
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Bury them in the ground! Send them to the place where dead people are, where they will not be able to get out!
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
After you do that, I will congratulate/praise you and say that [truly] you can save yourself by your own ability/power.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
“Think [also] about the huge animals that live near the water. I made you, and I made them also. They eat grass, like oxen do.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Their legs/thighs are [very] strong, and the muscles of their bellies are [very] powerful.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
Their tails are stiff (OR, bend down) like the branches of a cedar tree. The sinews/muscles of their thighs are close together.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
Their [thigh] bones are [like] tubes [made] of bronze, and the bones of their legs are like bars [made] of iron.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
They are among the strongest of the animals that I made, and I, who created them, am the only one who can kill them.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
On the hills grows food [PRS] for them to eat while many [HYP] other wild animals play nearby.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
They lie down [in the water] under the lotus plants; they hide in [tall] reeds in the swamps.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
Those huge animals find shade under the lotus plants, and they are surrounded by poplar trees.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
They are not disturbed by raging/swiftly-flowing rivers; they are not even disturbed/frightened when [rivers like the] Jordan [River] rush over them.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
No one can [RHQ] catch them by blinding their eyes or by piercing their noses with [the teeth of] a trap!”

< Ayubu 40 >