< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
Moreover the LORD answered Job, and said,
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
Shall he that contends with the Almighty instruct him? he that reproves God, let him answer it.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Then Job answered the LORD, and said,
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
Behold, I am vile; what shall I answer you? I will lay mine hand upon my mouth.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
Once have I spoken; but I will not answer: yea, twice; but I will proceed no further.
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
Then answered the LORD unto Job out of the whirlwind, and said,
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gird up your loins now like a man: I will demand of you, and declare you unto me.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Will you also nullify my judgment? will you condemn me, that you may be righteous?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Have you an arm like God? or can you thunder with a voice like him?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Deck yourself now with majesty and excellency; and array yourself with glory and beauty.
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Cast abroad the rage of your wrath: and behold every one that is proud, and bring low him.
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Look on every one that is proud, and bring him low; and tread down the wicked in their place.
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Hide them in the dust together; and bind their faces in secret.
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
Then will I also confess unto you that your own right hand can save you.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
Behold now behemoth, which I made with you; he eats grass as an ox.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Lo now, his strength is in his loins, and his force is in the navel of his belly.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
He moves his tail like a cedar: the sinews of his stones are wrapped together.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
His bones are as strong pieces of brass; his bones are like bars of iron.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
He is the chief of the ways of God: he that made him can make his sword to approach unto him.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
Surely the mountains bring him forth food, where all the beasts of the field play.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
He lies under the shady trees, in the covert of the reed, and fens.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
The shady trees cover him with their shadow; the willows of the brook compass him about.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
Behold, he drinks up a river, and hastes not: he trusts that he can draw up Jordan into his mouth.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
He takes it with his eyes: his nose pierces through snares.

< Ayubu 40 >