< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
And the LORD said to Job:
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
“Will the faultfinder contend with the Almighty? Let him who argues with God give an answer.”
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Then Job answered the LORD:
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
“Behold, I am insignificant. How can I reply to You? I place my hand over my mouth.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
I have spoken once, but I have no answer— twice, but I have nothing to add.”
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
Then the LORD answered Job out of the whirlwind and said:
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
“Now brace yourself like a man; I will question you, and you shall inform Me.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Would you really annul My justice? Would you condemn Me to justify yourself?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Do you have an arm like God’s? Can you thunder with a voice like His?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Then adorn yourself with majesty and splendor, and clothe yourself with honor and glory.
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Unleash the fury of your wrath; look on every proud man and bring him low.
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Look on every proud man and humble him; trample the wicked where they stand.
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Bury them together in the dust; imprison them in the grave.
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
Then I will confess to you that your own right hand can save you.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
Look at Behemoth, which I made along with you. He feeds on grass like an ox.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
See the strength of his loins and the power in the muscles of his belly.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
His tail sways like a cedar; the sinews of his thighs are tightly knit.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
His bones are tubes of bronze; his limbs are rods of iron.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
He is the foremost of God’s works; only his Maker can draw the sword against him.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
The hills yield him their produce, while all the beasts of the field play nearby.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
He lies under the lotus plants, hidden among the reeds of the marsh.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
The lotus plants conceal him in their shade; the willows of the brook surround him.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
Though the river rages, Behemoth is unafraid; he remains secure, though the Jordan surges to his mouth.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
Can anyone capture him as he looks on, or pierce his nose with a snare?

< Ayubu 40 >