< Ayubu 40 >

1 Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
En de HEERE antwoordde Job, en zeide:
2 “Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
Is het twisten met den Almachtige onderrichten? Wie God bestraft, die antwoorde daarop.
3 Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
Toen antwoordde Job den HEERE, en zeide:
4 Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
Zie, ik ben te gering; wat zou ik U antwoorden? Ik leg mijn hand op mijn mond.
5 Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
Eenmaal heb ik gesproken, maar zal niet antwoorden; of tweemaal, maar zal niet voortvaren.
6 Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
En de HEERE antwoordde Job uit een onweder, en zeide:
7 “Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Gord nu als een man uw lenden; Ik zal u vragen, en onderricht Mij.
8 Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
Zult gij ook Mijn oordeel te niet maken? Zult Gij Mij verdoemen, opdat gij rechtvaardig zijt?
9 Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
Hebt gij een arm gelijk God? En kunt gij, gelijk Hij, met de stem donderen?
10 Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
Versier u nu met voortreffelijkheid en hoogheid, en bekleed u met majesteit en heerlijkheid!
11 Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
Strooi de verbolgenheden uws toorns uit, en zie allen hoogmoedige, en verneder hem!
12 Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
Zie allen hoogmoedige, en breng hem ten onder; en verpletter de goddelozen in hun plaats!
13 Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
Verberg hen te zamen in het stof; verbind hun aangezichten in het verborgen!
14 Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
Dan zal Ik ook u loven, omdat uw rechterhand u zal verlost hebben.
15 Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
Zie nu Behemoth, welken Ik gemaakt heb nevens u; hij eet hooi, gelijk een rund.
16 Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
Zie toch, zijn kracht is in zijn lenden, en zijn macht in den navel zijns buiks.
17 Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
Als het hem lust, zijn staart is als een ceder; de zenuwen zijner schaamte zijn doorvlochten.
18 Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
Zijn beenderen zijn als vast koper; zijn gebeenten zijn als ijzeren handbomen.
19 Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
Hij is een hoofdstuk der wegen Gods; Die hem gemaakt heeft, heeft hem zijn zwaard aangehecht.
20 Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
Omdat de bergen hem voeder voortbrengen, daarom spelen al de dieren des velds aldaar.
21 Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
Onder schaduwachtige bomen ligt hij neder, in een schuilplaats des riets en des slijks.
22 Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
De schaduwachtige bomen bedekken hem, elkeen met zijn schaduw; de beekwilgen omringen hem.
23 Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
Zie, hij doet de rivier geweld aan, en verhaast zich niet; hij vertrouwt, dat hij de Jordaan in zijn mond zou kunnen intrekken.
24 Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?
Zou men hem voor zijn ogen kunnen vangen? Zou men hem met strikken den neus doorboren kunnen?

< Ayubu 40 >