< Ayubu 39 >
1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
¿Sabes tú cuándo paren las cabras monteses? ¿Asististe al parto de las venadas?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
¿Puedes contar los meses de su preñez y saber el tiempo cuando paren?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
Se encorvan, expulsan sus crías, se libran de sus dolores de parto.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Sus crías crecen, se fortalecen, salen a campo abierto y no vuelven.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
¿Quién dio al asno montés su libertad? ¿Quién soltó las ataduras del rebuznante,
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
a cual di el desierto como hogar y tierra salitrosa como vivienda?
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
Se burla del bullicio de la ciudad y no obedece los gritos del arriero,
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
explora las montañas en busca de su pasto y rastrea toda cosa verde.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
¿Consentirá el búfalo en ser tu esclavo o pasará la noche en tu establo?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
¿Atarás al búfalo al arado con cuerdas? ¿Rastrillará los valles tras ti?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
¿Confiarás en él porque es robusto y dejarás tu labor a su cuidado?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
¿Confiarás en él para que te traiga tu cosecha y reúna el grano en tu era?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
Las alas del avestruz se agitan alegres, ¿pero son las alas y el plumaje del amor?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
Abandona sus huevos en la tierra, en el polvo los calienta
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
y se olvida que un pie puede aplastarlos o una bestia salvaje pisotearlos.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
Es cruel con sus polluelos como si no fueran suyos. No le importa que se pierda su fatiga,
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
porque ʼEloah lo privó de sabiduría y no lo dotó de entendimiento.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
Pero cuando se yergue en alto, se burla del caballo y su jinete.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
¿Diste al caballo su fuerza? ¿Cubriste tú su cuello con una melena?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
¿Lo harás brincar como langosta? Su majestuoso resoplido es terrible,
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
escarba en el valle, se regocija en su fuerza, sale a encontrarse con las armas,
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
se ríe del miedo y no se espanta ni retrocede ante la espada.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
La flecha resuena contra él. Fulguran lanzas y arma arrojadiza,
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
con ímpetu y furor devora la distancia, sin que le importe el sonido de la trompeta.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
Parece que dice entre clarines: ¡Ea! Olfatea desde lejos la batalla, el grito de los comandantes y el grito de guerra.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
¿Vuela el halcón y extiende sus alas hacia el sur por tu sabiduría?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
¿Por tu mandato se remonta el águila y pone su nido en la altura?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
Vive y tiene su habitación en la roca, en la cumbre del peñasco, en lugar inaccesible.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
Desde allí acecha la presa. Sus ojos la divisan desde muy lejos.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
Sus polluelos chupan la sangre. Donde hay carroña, allí está ella.