< Ayubu 39 >
1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
“¿Sabéis en qué momento paren las cabras montesas? ¿Observas cuando la cierva tiene cervatillo?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
¿Puedes contar los meses que cumplen? ¿O sabes la hora en que dan a luz?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
Se inclinan. Llevan a sus crías. Terminan sus dolores de parto.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Sus crías se hacen fuertes. Crecen en el campo abierto. Salen y no vuelven.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
“¿Quién ha liberado al burro salvaje? O que ha soltado las amarras del asno veloz,
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
cuyo hogar he convertido en el desierto, y la tierra salada su morada?
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
Desprecia el tumulto de la ciudad, tampoco oye los gritos del conductor.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
La cordillera es su pasto. Busca cada cosa verde.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
“¿Se contentará el buey salvaje con servirte? ¿O se quedará junto a tu comedero?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
¿Puedes sujetar al buey salvaje en el surco con su arnés? ¿O va a labrar los valles después de ti?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
¿Confiarás en él, porque su fuerza es grande? ¿O le dejarás tu trabajo?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
¿Confiarás en él para que traiga a casa tu semilla? y recoger el grano de tu era?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
“Las alas del avestruz se agitan con orgullo, ¿pero son las plumas y el plumaje del amor?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
Porque deja sus huevos en la tierra, los calienta en el polvo,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
y olvida que el pie puede aplastarlos, o que el animal salvaje los pisotee.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
Trata con dureza a sus crías, como si no fueran suyas. Aunque su trabajo es en vano, no tiene miedo,
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
porque Dios la ha privado de sabiduría, tampoco le ha impartido entendimiento.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
Cuando se eleva a lo alto, desprecia al caballo y a su jinete.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
“¿Le has dado fuerza al caballo? ¿Has vestido su cuello con una melena temblorosa?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
¿Le has hecho saltar como una langosta? La gloria de su resoplido es impresionante.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
Pisa el valle y se regocija en su fuerza. Sale al encuentro de los hombres armados.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
Se burla del miedo y no se amilana, ni se aparta de la espada.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
El carcaj se sacude contra él, la lanza y la jabalina.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
Come la tierra con fiereza y rabia, ni se queda quieto al sonido de la trompeta.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
Cada vez que suena la trompeta, resopla: “¡Ah! Huele la batalla a lo lejos, el estruendo de los capitanes, y los gritos.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
“¿Es por tu sabiduría que el halcón vuela, y extiende sus alas hacia el sur?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
¿Es por tu orden que el águila se levanta, y hace su nido en las alturas?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
En el acantilado habita y hace su hogar, en la punta del acantilado y la fortaleza.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
Desde allí espía la presa. Sus ojos lo ven de lejos.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
Sus crías también chupan sangre. Donde están los muertos, allí está él”.