< Ayubu 39 >
1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
Czy znasz porę, kiedy rodzą górskie kozice? Czy wiesz, kiedy rodzą łanie?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Czy możesz zliczyć miesiące, w których noszą [młode]? Czy znasz czas ich porodu?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
Przykucają, rodzą swoje młode, pozbywają się ich z bólem;
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Ich młode wzmacniają się, rosną wśród zboża, odchodzą i już do nich nie wracają.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Kto wypuścił dzikiego osła na wolność i kto rozwiązał jego pęta?
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
[Za] dom dałem mu pustynię, a [za] jego mieszkanie słone miejsca.
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
On naśmiewa się ze zgiełku miejskiego i nie słucha głosu poganiacza.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
Wypatruje w górach paszy i szuka wszelkiej zielonej trawy.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
Czy jednorożec zechce ci służyć albo nocować przy twoim żłobie?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
Czy możesz powrozem zaprzęgać jednorożca do bruzdy? Czy będzie bronował doliny za tobą?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
Czy zaufasz mu, ponieważ jego siła jest wielka? Czy powierzysz mu swoją pracę?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
Czy zawierzysz mu, że zwiezie twoje ziarno i zgromadzi je w twoim spichlerzu?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
Czy [dałeś] pawiowi piękne skrzydła, a skrzydła i pióra strusiowi?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
Składa swoje jaja na ziemię i ogrzewa je w prochu;
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
I zapomina, że noga może je rozgnieść lub dzikie zwierzę może zdeptać.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
Jest twardy [dla] swoich młodych, [jakby] nie [były] jego. Nie boi się, że jego trud jest próżny;
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
Bo Bóg pozbawił go mądrości i nie udzielił mu rozumu.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
Kiedy jednak podnosi się wysoko, naśmiewa się z konia i z jego jeźdźca.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Czy możesz dać koniowi moc? Czy rżeniem ozdobiłeś jego szyję?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
Czy przestraszysz go jak szarańczę? Parskanie jego nozdrzy [jest] straszne.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
Grzebie [kopytem] w ziemi i cieszy się [swą] siłą, biegnie przeciwko uzbrojonym.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
Drwi sobie z lęku i nie boi się, i nie ustępuje przed ostrzem miecza.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
Kołczan na nim chrzęści, błyszczy oszczep i dzida.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
Z grzmotem i z gniewem pochłania ziemię i nie staje spokojnie na głos trąby.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
Na głos trąby mówi: Ha, ha; z daleka czuje bitwę, grom dowódców i okrzyk.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
Czy dzięki twojemu rozumowi lata jastrząb [i] rozciąga swe skrzydła ku południu?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
Czy na twój rozkaz orzeł wzbija się i zakłada swoje gniazdo wysoko?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
Mieszka na skale, przebywa na iglicach jak na zamku.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
Stamtąd wypatruje [sobie] pokarmu, jego oczy widzą daleko.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
Jego młode też piją krew, a gdzie są zabici, tam jest on.