< Ayubu 39 >
1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
¿ Do you know [the] time of [the] bringing forth of mountain goats of rock [the] giving birth of does do you watch?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Will you count? [the] months [which] they complete and do you know? [the] time of bringing forth they.
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
They kneel down young their they cleave open labor-pains their they send forth.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
They become strong young their they grow in the open they go forth and not they return to them.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Who? did he let loose [the] wild donkey free and [the] fetters of [the] wild ass who? did he loosen.
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
Which I appointed [the] desert plain home its and dwelling-places its [the] saltiness.
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
It laughs to [the] tumult of a town [the] shouting of a driver not it hears.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
It explores mountains pasture its and after every green plant it searches.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
¿ Is it willing a wild ox to serve you or? will it pass [the] night at feeding trough your.
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
¿ Will you bind [the] wild ox in a furrow rope its or? will it harrow valleys behind you.
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
¿ Will you trust in it for [is] great strength its so you may leave? to it toil your.
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
¿ Will you trust in it that (it will bring back *Q(K)*) seed your and threshing floor your it will gather.
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
[the] wing of Ostriches it flaps joyously if a pinion a stork and plumage.
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
For it abandons to the ground eggs its and on [the] dust it keeps [them] warm.
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
And it has forgotten that a foot it will crush it and [the] animal of the field it will trample it.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
It treats roughly young its to not [belonging] to it [is] to emptiness labor its not fear.
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
For he has made forget it God wisdom and not he gave a share to it in understanding.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
About the time on the height it flaps it laughs to the horse and to rider its.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
¿ Do you give to the horse strength ¿ do you clothe neck its a mane.
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
¿ Do you make leap it like locust [the] majesty of snorting its [is] terror.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
They paw in the valley so it may rejoices in strength it goes forth to meet weaponry.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
It laughs to fear and not it is dismayed and not it turns back from before a sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
On it it rattles a quiver [the] blade of a spear and a javelin.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
With shaking and excitement it swallows [the] ground and not it stands firm for [the] sound of a horn.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
In [the] sufficiency of a horn - it says aha! and from a distance it smells battle [the] thunder of commanders and [the] battle-cry.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
¿ From understanding your does it soar a falcon does it spread out? (wings its *Q(K)*) to [the] south.
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
Or? on mouth your does it make high [its flight] an eagle and that it sets on high nest its.
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
A rock it dwells and it may pass [the] night on [the] tooth of a rock and a stronghold.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
From there it spies out food from afar eyes its they look.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
(And young ones its *Q(K)*) they drink blood and at where [those] slain [are] [is] there it.