< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
Knowest thou the time when the wild goats of the rock bring forth? Or canst thou observe when the hinds are in labor?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Canst thou number the months they fulfill, And know the season when they bring forth?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
They bow themselves; they bring forth their young; They cast forth their pains.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Their young ones are strong; they grow up in the fields; They go away, and return not to them.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Who hath sent forth the wild ass free? Who hath loosed the bands of the wild ass,
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
To whom I have given the wilderness for his house, And the barren land for his dwelling-place?
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
He scorneth the tumult of the city, And heedeth not the shouting of the driver;
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
The range of the mountains is his pasture; He seeketh after every green thing,
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
Will the wild-ox consent to serve thee? Will he pass the night at thy crib?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
Canst thou bind the wild-ox with the harness to the furrow? Or will he harrow the valleys after thee?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
Wilt thou rely upon him because his strength is great, And commit to him thy labor?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
Wilt thou trust him to bring home thy grain, And gather in thy harvest?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
The wing of the ostrich moveth joyfully; But is it with loving pinion and feathers?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
Nay, she layeth her eggs on the ground; She warmeth them in the dust,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
And forgetteth that the foot may crush them, And that the wild beast may break them.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
She is cruel to her young, as if they were not hers; Her labor is in vain, yet she feareth not;
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
Because God hath denied her wisdom, And hath not given her understanding.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
Yet when she lasheth herself up on high, She laugheth at the horse and his rider.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Hast thou given the horse strength? Hast thou clothed his neck with his trembling mane?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
Hast thou taught him to bound like the locust? How majestic his snorting! how terrible!
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
He paweth in the valley; he exulteth in his strength, And rusheth into the midst of arms.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
He laugheth at fear; he trembleth not, And turneth not back from the sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
Against him rattle the quiver, The flaming spear, and the lance.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
With rage and fury he devoureth the ground; He will not believe that the trumpet soundeth.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
At every blast of the trumpet, he saith, Aha! And snuffeth the battle afar off, —The thunder of the captains, and the war-shout.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
Is it by thy wisdom that the hawk flieth, And spreadeth his wings toward the south?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
Doth the eagle soar at thy command, And build his nest on high?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
He dwelleth and lodgeth upon the rock, Upon the peak of the rock, and the stronghold.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
From thence he spieth out prey; His eyes discern it from afar.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
His young ones suck up blood; And where the slain are, there is he.

< Ayubu 39 >