< Ayubu 39 >

1 Je unajua ni wakati gani mbuzi mwitu huzaa watoto wao katika miamba? Je waweza kuwangalia paa wakati wanapozaa watoto wao?
Knowest thou the time when the wild goats of the rock bring forth? [Or] canst thou mark when the hinds do calve?
2 Waweza kuhesabu miezi ya kuchukua mimba? Je unaujua muda ambao huzaa watoto wao?
Canst thou number the months that they fulfil? Or knowest thou the time when they bring forth?
3 Wanainama chini na kuzaa watoto wao, na kisha maumivu yao ya uzazi yanaishi.
They bow themselves, they bring forth their young, They cast out their pains.
4 Watoto wao huwa na nguvu na kukua katika uwanda wa wazi; hutoka nje na hawarudi tena.
Their young ones become strong, they grow up in the open field; They go forth, and return not again.
5 Ni nani huwaacha punda mwitu waende huru? Je nani amevilegeza vifungo vya punda wepesi,
Who hath sent out the wild ass free? Or who hath loosed the bonds of the swift ass,
6 ni nyumba ya nani nimeifanya katika Araba, au nyumba yake katika nchi ya chumvi?
Whose home I have made the wilderness, And the salt land his dwelling-place?
7 Hucheka kwa dharau katika kelele katika mji; hasikilizi kelele za mwongozaji.
He scorneth the tumult of the city, Neither heareth he the shoutings of the driver.
8 Hutembeatembea juu ya milima kama malisho yake; huko hutafuta kila mmea ulio wa kijani kwa ajili ya kula.
The range of the mountains is his pasture, And he searcheth after every green thing.
9 Je nyati atakuwa na furaha kukutumikia? Je atakubali kukaa katika zizi lako?
Will the wild-ox be content to serve thee? Or will he abide by thy crib?
10 Waweza kumwongoza nyati kulima mtaro kwa kamba? Je atachimba bonde kwa ajili yako?
Canst thou bind the wild-ox with his band in the furrow? Or will he harrow the valleys after thee?
11 Je waweza kumtumaini kwasababu ya nguvu zake nyingi? Je waweza kumwachia kazi yako ili aifanye?
Wilt thou trust him, because his strength is great? Or wilt thou leave to him thy labor?
12 Je waweza kumtegemea akuletee nyumbani nafaka, au kukusanya nafaka katika uwanda wako wa kupuria?
Wilt thou confide in him, that he will bring home thy seed, And gather [the grain] of thy threshing-floor?
13 Mabawa ya mbuni hupunga kwa majivuno, bali je mabawa na manyoya yana upendo?
The wings of the ostrich wave proudly; [But] are they the pinions and plumage of love?
14 Kwa maana huuacha mayai yake katika nchi, na huyaacha yapate joto katika mavumbi;
For she leaveth her eggs on the earth, And warmeth them in the dust,
15 husahau kuwa mguu waweza kuyaharibu au kwamba mnyama mwitu aweza kuyakanyaga.
And forgetteth that the foot may crush them, Or that the wild beast may trample them.
16 Huyatendea vibaya makinda yake kana kwamba si yake; haogopi kwamba kazi yake yaweza kupotea bure,
She dealeth hardly with her young ones, as if they were not hers: Though her labor be in vain, [she is] without fear;
17 kwasababu Mungu amemnyima hekima na hajampa ufahamu wowote.
Because God hath deprived her of wisdom, Neither hath he imparted to her understanding.
18 Na wakati anapokimbia kwa haraka, huwacheka kwa dharau farasi na mpanda farasi wake.
What time she lifteth up herself on high, She scorneth the horse and his rider.
19 Je umempa farasi nguvu zake? Je umeivika shingo yake kwa manyoya?
Hast thou given the horse [his] might? Hast thou clothed his neck with the quivering mane?
20 Je umemfanya aruke kama panzi? Enzi ya mlio wake ni wa kutisha.
Hast thou made him to leap as a locust? The glory of his snorting is terrible.
21 Hurarua kwa nguvu na kufurahia katika nguvu zake; hukimbia upesi kukutana na silaha.
He paweth in the valley, and rejoiceth in his strength: He goeth out to meet the armed men.
22 Huidharau hofu na hashangazwi; huwa harudi nyuma kutoka katika upanga.
He mocketh at fear, and is not dismayed; Neither turneth he back from the sword.
23 Podo hugongagonga ubavuni mwake, pamoja na mkuki unaong'aa na fumo.
The quiver rattleth against him, The flashing spear and the javelin.
24 Huimeza nchi kwa hasira na ghadhabu; katika sauti ya tarumbeta, hawezi kusimama sehemu moja.
He swalloweth the ground with fierceness and rage; Neither believeth he that it is the voice of the trumpet.
25 Wakati wowote tarumbeta inapolia, husema, 'Ooh! Huisikia harufu ya vita kutoka mbali - vishindo vya radi za makamanda na makelele.
As oft as the trumpet [soundeth] he saith, Aha! And he smelleth the battle afar off, The thunder of the captains, and the shouting.
26 Je ni kwa hekima yako kwamba mwewe hupaa juu, na ya kuwa huyanyosha mabawa yake kwa upande wa kusini?
Is it by thy wisdom that the hawk soareth, [And] stretcheth her wings toward the south?
27 Je ni kwa agizo lako kwamba tai huruka juu na kufanya kiota chake katika sehemu za juu?
Is it at thy command that the eagle mounteth up, And maketh her nest on high?
28 Huishi katika majabali na hufanya makao yake katika vilele vya majabali, na ngomeni.
On the cliff she dwelleth, and maketh her home, Upon the point of the cliff, and the stronghold.
29 Kutoka huko hutafuta mawindo; macho yake huyaona mawindo kutoka mbali.
From thence she spieth out the prey; Her eyes behold it afar off.
30 Makinda yake hunywa damu pia; na pale walipo watu wafu, ndipo na yeye alipo.
Her young ones also suck up blood: And where the slain are, there is she.

< Ayubu 39 >