< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Entonces Yahvé respondió a Job desde el torbellino,
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
“¿Quién es el que oscurece el consejo por palabras sin conocimiento?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Prepárate como un hombre, porque yo te interrogaré y tú me responderás.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
“¿Dónde estabas cuando puse los cimientos de la tierra? Declara, si tienes entendimiento.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
¿Quién determinó sus medidas, si lo sabe? ¿O quién estiró la línea en él?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
¿Sobre qué estaban fijados sus cimientos? O quién puso su piedra angular,
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
cuando las estrellas de la mañana cantaban juntas, y todos los hijos de Dios gritaron de alegría?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
“O que cierra el mar con puertas, cuando salió del vientre materno,
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
cuando hice de las nubes su vestimenta, y lo envolvió en una espesa oscuridad,
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
marcadas para ello mi límite, poner barras y puertas,
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
y dijo: “Puedes venir aquí, pero no más allá. ¿Tus orgullosas olas serán detenidas aquí?
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
“¿Has ordenado la mañana en tus días, y ha hecho que el amanecer conozca su lugar,
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
para que se apodere de los confines de la tierra, y sacudir a los malvados fuera de ella?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Se cambia como la arcilla bajo el sello, y presentado como una prenda de vestir.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
A los malvados se les oculta la luz. El brazo alto está roto.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
“¿Has entrado en los manantiales del mar? ¿O has caminado por los recovecos de las profundidades?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
¿Se te han revelado las puertas de la muerte? ¿O has visto las puertas de la sombra de la muerte?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
¿Has comprendido la tierra en su anchura? Declara, si lo sabes todo.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
“¿Cuál es el camino hacia la morada de la luz? En cuanto a la oscuridad, cuál es su lugar,
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
que lo lleves a su límite, para que discierna los caminos de su casa?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Seguramente lo sabes, pues naciste entonces, ¡y el número de sus días es genial!
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
¿Has entrado en los almacenes de la nieve, o has visto los almacenes del granizo,
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
que he reservado para el tiempo de la angustia, contra el día de la batalla y la guerra?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
De qué manera se distribuye el rayo, o el viento del este disperso en la tierra?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Que ha cortado un canal para el agua de la inundación, o la trayectoria de la tormenta,
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
para hacer llover en una tierra donde no hay hombre, en el desierto, en el que no hay hombre,
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
para saciar el terreno baldío y desolado, para hacer crecer la hierba tierna?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
¿La lluvia tiene padre? ¿O quién recoge las gotas de rocío?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
¿De qué vientre salió el hielo? ¿Quién ha dado a luz a la escarcha gris del cielo?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Las aguas se vuelven duras como la piedra, cuando la superficie de las profundidades está congelada.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
“¿Puedes atar el cúmulo de las Pléyades, o aflojar las cuerdas de Orión?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
¿Puedes guiar a las constelaciones en su estación? ¿O puedes guiar a la Osa con sus cachorros?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
¿Conoces las leyes de los cielos? ¿Puede establecer su dominio sobre la tierra?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
“¿Puedes elevar tu voz a las nubes, para que la abundancia de aguas te cubra?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
¿Puedes enviar relámpagos para que se vayan? ¿Te informan de que “aquí estamos”?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
¿Quién ha puesto la sabiduría en las partes interiores? ¿O quién ha dado entendimiento a la mente?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
¿Quién puede contar las nubes con sabiduría? O que puede verter los contenedores del cielo,
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
cuando el polvo se convierte en una masa, y los terrones se pegan?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
“¿Puedes cazar la presa para la leona, o satisfacer el apetito de los jóvenes leones,
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
cuando se agazapan en sus guaridas, y acechar en la espesura?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Que proporciona al cuervo su presa, cuando sus jóvenes claman a Dios, y vagan por falta de comida?

< Ayubu 38 >