< Ayubu 38 >
1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
Potem PAN odpowiedział Hiobowi spośród wichru:
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
Kim jest ten, co zaciemnia radę słowami bez poznania?
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
Przepasz teraz swe biodra jak mężczyzna, będę cię pytał, a ty mi odpowiadaj.
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
Gdzie byłeś, kiedy zakładałem fundamenty ziemi? Powiedz, jeśli masz [tę] wiedzę.
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
Kto określił jej rozmiary? Czy wiesz? Kto rozciągnął nad nią sznur?
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
Na czym są oparte jej podstawy? Kto położył jej kamień węgielny;
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
Gdy gwiazdy poranne razem śpiewały i radowali się wszyscy synowie Boży?
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
Kto zamknął bramą morze, gdy się wyrywało [jakby] wychodzące z łona?
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
Gdy chmurę uczyniłem jego szatą, a ciemność jego pieluszkami;
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
Gdy ustanowiłem o nim swój dekret i poustawiałem rygle i bramy;
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
I powiedziałem: Dotąd dojdziesz, a nie dalej; tu położysz swe nadęte fale.
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
Czy kiedykolwiek w swoim życiu rozkazywałeś rankowi i wskazałeś zorzy jej miejsce;
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
Aby ogarnęła krańce ziemi i aby niegodziwi zostali z niej strząśnięci?
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
Ona zmienia się jak glina pod pieczęcią, [a wszystko] stoi jak szata.
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
Niegodziwym jest odebrana ich światłość, a wyniosłe ramię będzie złamane.
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
Czy dotarłeś aż do źródeł morza? Czy przechadzałeś się po dnie głębin?
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
Czy bramy śmierci zostały przed tobą odkryte? Czy widziałeś bramy cienia śmierci?
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
Czy pojąłeś szerokość ziemi? Powiedz mi, jeśli to wszystko wiesz.
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
Gdzie jest droga do miejsca przebywania światłości? Gdzie swoje miejsce [ma] ciemność;
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
Abyś ją zaprowadził do jej granic i mógł poznać ścieżki do jej domu?
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
Czy wiesz to, bo wtedy się urodziłeś i liczba twoich dni [jest] wielka?
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
Czy dotarłeś do skarbnic śniegu? Czy widziałeś skarbnice gradu;
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
Który zachowuję na czas ucisku, na dzień bitwy i wojny?
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
Jaką drogą dzieli się światłość, która rozpędza wiatr wschodni po ziemi?
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
Kto podzielił kanał dla ulewy i drogę dla błyskawicy grzmotu;
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
Aby padał deszcz na ziemię, w której nikt nie mieszka, i na pustynię, gdzie nie ma człowieka;
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
Aby nasycił [miejsce] puste i jałowe oraz zasilił rosnącą [tam] trawę?
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
Czy deszcz ma ojca? A kto spłodził krople rosy?
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
Z czyjego łona wychodzi lód? A kto spłodził szron niebieski?
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
Wody zostają przykryte niczym kamieniem, gdy powierzchnia głębiny zamarza.
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
Czy możesz związać jasne gwiazdy Plejad albo rozluźnić więzy Oriona?
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
Czy wyprowadzisz w swym czasie gwiazdy południowe? Czy poprowadzisz Niedźwiedzicę z jej synami?
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
Czy znasz porządek nieba? Czy możesz ustanowić jego panowanie na ziemi?
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
Czy podniesiesz swój głos ku chmurom, aby cię ulewa przykryła?
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
Czy możesz wypuścić błyskawice, aby przyszły i mówiły: Oto jesteśmy?
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
Kto włożył we wnętrze [ludzkie] mądrość? Kto dał sercu rozum?
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
Kto zdoła policzyć chmury [swoją] mądrością? Kto uspokoi, kiedy leje z nieba;
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
Gdy proch twardnieje, a bryły przylegają do siebie?
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
Czy lwu zdobyczy nałowisz, czy zaspokoisz głód lwiątek;
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
Gdy tulą się w swoich jaskiniach i czyhają w cieniu swoich jam?
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
Kto dostarcza krukowi pokarmu, gdy jego młode wołają do Boga [i] tułają się bez pożywienia?