< Ayubu 38 >

1 Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
و خداوند ایوب را از میان گردبادخطاب کرده، گفت:۱
2 “Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
«کیست که مشورت را از سخنان بی‌علم تاریک می‌سازد؟۲
3 Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
الان کمر خود را مثل مرد ببند، زیرا که از توسوال می‌نمایم پس مرا اعلام نما.۳
4 Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
وقتی که زمین را بنیاد نهادم کجا بودی؟ بیان کن اگر فهم داری.۴
5 Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
کیست که آن را پیمایش نمود؟ اگر می‌دانی! وکیست که ریسمانکار را بر آن کشید؟۵
6 Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
پایه هایش بر چه چیز گذاشته شد؟ و کیست که سنگ زاویه‌اش را نهاد،۶
7 wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
هنگامی که ستارگان صبح باهم ترنم نمودند، و جمیع پسران خدا آوازشادمانی دادند؟۷
8 Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
و کیست که دریا را به درهامسدود ساخت، وقتی که به در جست و از رحم بیرون آمد؟۸
9 wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
وقتی که ابرها را لباس آن گردانیدم و تاریکی غلیظ را قنداقه آن ساختم.۹
10 Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
و حدی برای آن قرار دادم و پشت بندها و درها تعیین نمودم.۱۰
11 na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
و گفتم تا به اینجا بیا و تجاوز منما. و دراینجا امواج سرکش تو بازداشته شود.۱۱
12 Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
«آیا تو از ابتدای عمر خود صبح را فرمان دادی، و فجر را به موضعش عارف گردانیدی؟۱۲
13 ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
تا کرانه های زمین را فرو‌گیرد و شریران از آن افشانده شوند.۱۳
14 Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
مثل گل زیر خاتم مبدل می‌گردد. و همه‌چیز مثل لباس صورت می‌پذیرد.۱۴
15 'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
و نور شریران از ایشان گرفته می‌شود، و بازوی بلند شکسته می‌گردد.۱۵
16 Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
آیا به چشمه های دریا داخل شده، یا به عمقهای لجه رفته‌ای؟۱۶
17 Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
آیا درهای موت برای تو باز شده است؟ یا درهای سایه موت را دیده‌ای؟۱۷
18 Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
آیاپهنای زمین را ادراک کرده‌ای؟ خبر بده اگر این همه را می‌دانی.۱۸
19 Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
راه مسکن نور کدام است، ومکان ظلمت کجا می‌باشد،۱۹
20 Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
تا آن را به حدودش برسانی، و راههای خانه او را درک نمایی؟۲۰
21 Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
البته می‌دانی، چونکه در آنوقت مولودشدی، و عدد روزهایت بسیار است!۲۱
22 Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
«آیا به مخزن های برف داخل شده، و خزینه های تگرگ را مشاهده نموده‌ای،۲۲
23 vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
که آنهارا به جهت وقت تنگی نگاه داشتم، به جهت روزمقاتله و جنگ؟۲۳
24 Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
به چه طریق روشنایی تقسیم می‌شود، و باد شرقی بر روی زمین منتشرمی گردد؟۲۴
25 Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
کیست که رودخانه‌ای برای سیل کند، یا طریقی به جهت صاعقه‌ها ساخت.۲۵
26 na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
تا برزمینی که کسی در آن نیست ببارد و بر بیابانی که در آن آدمی نباشد،۲۶
27 kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
تا (زمین ) ویران و بایر راسیراب کند، و علفهای تازه را از آن برویاند؟۲۷
28 Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
آیا باران را پدری هست؟ یا کیست که قطرات شبنم را تولید نمود؟۲۸
29 Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
از رحم کیست که یخ بیرون آمد؟ و ژاله آسمان را کیست که تولیدنمود؟۲۹
30 Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
آبها مثل سنگ منجمد می‌شود، وسطح لجه یخ می‌بندد.۳۰
31 Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
آیا عقد ثریا رامی بندی؟ یا بندهای جبار را می‌گشایی؟۳۱
32 Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
آیابرجهای منطقه البروج را در موسم آنها بیرون می‌آوری؟ و دب اکبر را با بنات او رهبری می‌نمایی؟۳۲
33 Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
آیا قانون های آسمان را می‌دانی؟ یا آن را بر زمین مسلط می‌گردانی؟۳۳
34 Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
آیا آوازخود را به ابرها می‌رسانی تا سیل آبها تو رابپوشاند؟۳۴
35 Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
آیا برقها را می‌فرستی تا روانه شوند، و به تو بگویند اینک حاضریم؟۳۵
36 Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
کیست که حکمت را در باطن نهاد یا فطانت را به دل بخشید؟۳۶
37 Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
کیست که با حکمت، ابرها رابشمارد؟ و کیست که مشکهای آسمان را بریزد؟۳۷
38 wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
چون غبار گل شده، جمع می‌شود و کلوخها باهم می‌چسبند.۳۸
39 Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
آیا شکار را برای شیر ماده صید می‌کنی؟ و اشتهای شیر ژیان را سیرمی نمایی؟۳۹
40 wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
حینی که در ماوای خود خویشتن را جمع می‌کنند و در بیشه در کمین می‌نشینند؟۴۰
41 Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?
کیست که غذا را برای غراب آماده می‌سازد، چون بچه هایش نزد خدا فریاد برمی آورند، و به‌سبب نبودن خوراک آواره می‌گردند؟۴۱

< Ayubu 38 >